Bunge la Tanzania
Jamhuri ya Muungano ya Tanzania
Term | Session | Sitting | Sector | Ministry | Qn No | Date |
---|---|---|---|---|---|---|
2020-2025 | Session 18 | Sitting 4 | Information, Communication and Information Technology | Wizara ya Mawasiliano na Teknolojia ya Habari | 64 | 2025-01-31 |
Name
Festo Richard Sanga
Sex
Male
Party
CCM
Constituent
Makete
Primary Question
MHE. FESTO R. SANGA aliuliza: -
Je, Serikali haioni haja ya kuzuia usajili holela wa laini za simu mitaani kutokana na utapeli unaoendelea mitandaoni?
Name
Maryprisca Winfred Mahundi
Sex
Female
Party
CCM
Constituent
Special Seats
Answer
NAIBU WAZIRI WA MAWASILIANO NA TEKNOLOJIA YA HABARI alijibu: -
Mheshimiwa Spika, Serikali imeweka miongozo ya kusajili laini za simu kupitia Kanuni za Mawasiliano ya Kielektroniki na Posta. Miongozo hii inahakikisha kuwa laini zote zinasajiliwa kwa alama za vidole, hivyo kutokuwepo kwa mianya ya kusajili laini kiholela. Hata hivyo, wahalifu wa mtandaoni hutumia mbinu kwa kuwalaghai mawakala na watumiaji ili laini zilizokwishasajiliwa zitumike kwenye uhalifu.
Mheshimiwa Spika, Serikali kupitia TCRA na watoa huduma za mawasiliano inaendelea kudhibiti vitendo vya uhalifu kupitia njia zifuatazo: -
(i) Kutoa elimu kwa umma juu ya uhalifu mtandaoni na njia za kujilinda;
(ii) Kuhakiki taarifa za usajili kupitia namba *106#; na
(iii) Kutoa taarifa za uhalifu kupitia namba 15040, ili kuchukua hatua stahiki dhidi ya vitendo vya udanganyifu.
Copyright © Bunge Polis 2025. All Rights Reserved