Bunge la Tanzania
Jamhuri ya Muungano ya Tanzania
Term | Session | Sitting | Sector | Ministry | Qn No | Date |
---|---|---|---|---|---|---|
2020-2025 | Session 18 | Sitting 4 | Livestock , Fisheries, Agriculture, Food Security and Cooperatives | Wizara ya Kilimo | 65 | 2025-01-31 |
Name
Cecil David Mwambe
Sex
Male
Party
CCM
Constituent
Ndanda
Primary Question
MHE. CECIL D. MWAMBE aliuliza:-
Je, Serikali haioni kuwa uwepo wa aina nyingi za viuatilifu kwenye zao la korosho ni kuwachanganya wakulima?
Name
David Ernest Silinde
Sex
Male
Party
CCM
Constituent
Tunduma
Answer
NAIBU WAZIRI WA KILIMO alijibu:-
Mheshimiwa Spika, viuatilifu mbalimbali vimeidhinishwa katika kudhibiti visumbufu vya zao la korosho kulingana na aina za magonjwa yanayoathiri mimea. Viuatilifu hivyo, vimesajiliwa kwa majina tofauti ya kibiashara bila kuathiri viambata amilifu (Active Ingredients) vyenye uwezo wa kudhibiti vimelea na wadudu waharibifu katika zao hilo. Hivyo, zao la korosho linaonekana kuwa na viuatilifu vingi kutokana na majina ya kibiashara yanayotumika katika usajili.
Mheshimiwa Spika, Serikali kupitia Bodi ya Korosho Tanzania, TARI Naliendele, Mamlaka ya Afya ya Mimea na Viuatilifu Tanzania (TPHPA), Sekretarieti za Mikoa na wasambazaji wa viuatilifu imeendelea kutoa mafunzo kwa wafanyabiashara wa viuatilifu, Maafisa Ugani na wakulima kuhusu matumizi sahihi na salama ya viuatilifu, uhifadhi pamoja na viwango vya uzimuaji (Pesticide application rate), ili kuwezesha ufanisi wa viuatilifu vinavyosambazwa kwa wakulima.
Copyright © Bunge Polis 2025. All Rights Reserved