Bunge la Tanzania
Jamhuri ya Muungano ya Tanzania
Term | Session | Sitting | Sector | Ministry | Qn No | Date |
---|---|---|---|---|---|---|
2020-2025 | Session 18 | Sitting 4 | Industries and Trade | Wizara ya Viwanda na Biashara | 68 | 2025-01-31 |
Name
Aziza Sleyum Ally
Sex
Male
Party
CCM
Constituent
Special Seats
Primary Question
MHE. ATHUMAN A. MAIGE K.n.y. MHE. AZIZA S. ALLY aliuliza:-
Je, nini mkakati wa Serikali wa kutafuta soko la asali?
Name
Exaud Silaoneka Kigahe
Sex
Male
Party
CCM
Constituent
Mufindi Kaskazini
Answer
NAIBU WAZIRI WA VIWANDA NA BIASHARA alijibu:-
Mheshimiwa Spika, Serikali imekuwa na mkakati wa kutafuta soko la asali ambao unajumuisha mafunzo ya uzalishaji bora katika mnyororo wa thamani wa asali. Ujenzi wa viwanda vya pamoja (common facilities) vya uchakataji bora wa asali, utangazaji wa bidhaa za asali zinazozalishwa nchini katika maonesho ya ndani, kikanda na kimataifa na kujumuisha fursa ya asali ya Tanzania katika majadiliano ya nchi na nchi, kikanda na Kimataifa.
Mheshimiwa Spika, hatua hizo zimewezesha kampuni ndogo (SMEs) 46 zinazozalisha asali kuuza tani 337.3 katika masoko ya nje, hususan soko la Ulaya, ambapo nchi zinazonunua kwa wingi ni Ujerumani, Uholanzi na Poland, ikifuatiwa na Soko la Afrika Mashariki (EAC); Kenya, Rwanda na Uganda na katika Soko la SADC, ikiwemo nchi ya Botswana. Jumla ya mauzo katika masoko hayo kwa mwaka 2023 yalikuwa na thamani ya shilingi bilioni 2.0.
Copyright © Bunge Polis 2025. All Rights Reserved