Bunge la Tanzania
Jamhuri ya Muungano ya Tanzania
Term | Session | Sitting | Sector | Ministry | Qn No | Date |
---|---|---|---|---|---|---|
2020-2025 | Session 18 | Sitting 1 | Home Affairs | Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi | 7 | 2025-01-28 |
Name
Josephat Sinkamba Kandege
Sex
Male
Party
CCM
Constituent
Kalambo
Primary Question
MHE. JOSEPHAT S. KANDEGE aliuliza:-
Je, lini Serikali itaondoa usumbufu wa kupata vibali na gharama pale raia wa Tanzania wanapolazimika kushiriki shughuli za kijamii Nchini Zambia?
Name
Daniel Baran Sillo
Sex
Male
Party
CCM
Constituent
Babati Vijijini
Answer
NAIBU WAZIRI WA MAMBO YA NDANI YA NCHI alijibu:-
Mheshimiwa Spika, Serikali imefunga mifumo ya kielektroniki katika ngazi za Mikoa na Wilaya ili kurahisisha upatikanaji wa hati za safari (pasipoti) na hati za dharura za safari kwa lengo la kuwaondolea usumbufu raia wa Tanzania pale wanapohitaji hati hizo kwa ajili ya kushiriki shughuli za kijamii katika nchi jirani. Kwa raia wanaoishi ndani ya eneo lisilozidi kilometa 10 kutoka mpaka wa nchi yetu na nchi jirani na wananchi wanapokuwa na shughuli za dharura kama vile misiba na magonjwa, hupatiwa ruhusa maalum kuwawezesha kwenda umbali usiozidi kilomita 10 ili waweze kushiriki shughuli hizo.
Mheshimiwa Spika, aidha, kwa wale wanaoenda nchi jirani kwa ajili ya shughuli za kiuchumi, wanapaswa kufuata sheria na taratibu za nchi husika katika kulipia vibali vinavyoendana na shughuli wanazoenda kufanya. Ahsante.
Copyright © Bunge Polis 2025. All Rights Reserved