Bunge la Tanzania
Jamhuri ya Muungano ya Tanzania
Name
Josephat Sinkamba Kandege
Sex
Male
Party
CCM
Constituent
Kalambo
Primary Question
MHE. JOSEPHAT S. KANDEGE aliuliza:- Je, lini Serikali itaondoa usumbufu wa kupata vibali na gharama pale raia wa Tanzania wanapolazimika kushiriki shughuli za kijamii Nchini Zambia?
Supplementary Question 1
MHE. JOSEPHAT S. KANDEGE: Mheshimiwa Spika, pamoja na majibu mazuri ya Serikali ninaomba niulize maswali madogo kama ifuatavyo:
Mheshimiwa Spika, swali la kwanza; kwa mwananchi wa kawaida ambaye anaenda kushiriki shughuli za kijamii kutozwa kibali shilingi 20,000 ni gharama kubwa sana. Je, Serikali itakuwa tayari kupunguza tozo hizo ili walau iwe shilingi 5,000 au shilingi 2,000 ikiwezekana?
Mheshimiwa Spika, swali la pili; ninashukuru Serikali wamefunga vifaa vya kielektroniki, ninataka kujua katika Wilaya ambazo zimenufaika na Wilaya ya Kalambo ni miongoni mwao? Ahsante sana.
Name
Daniel Baran Sillo
Sex
Male
Party
CCM
Constituent
Babati Vijijini
Answer
NAIBU WAZIRI WA MAMBO YA NDANI YA NCHI: Mheshimiwa Spika, ninaomba kujibu maswali ya Mheshimiwa Kandege, kama ifuatavyo:-
Mheshimiwa Spika, tozo hizi za shilingi 20,000 zipo kwa mijibu wa sheria pale ambapo tutaona kuna haja ya kupunguza basi Serikali itayafanyia kazi mapendekezo ya Mheshimiwa Mbunge.
Mheshimiwa Spika, swali lake la pili, nadhani ameipongeza Serikali kuweka mifumo ya kielektroniki ambapo Wilaya ya Kalambo pia imenufaika. Ahsante sana.
Copyright © Bunge Polis 2025. All Rights Reserved