Bunge la Tanzania
Jamhuri ya Muungano ya Tanzania
Term | Session | Sitting | Sector | Ministry | Qn No | Date |
---|---|---|---|---|---|---|
2020-2025 | Session 18 | Sitting 1 | Information, Communication and Information Technology | Wizara ya Habari, Mawasiliano na Teknolojia ya Habari | 11 | 2025-01-28 |
Name
Oliver Daniel Semuguruka
Sex
Female
Party
CCM
Constituent
Special Seats
Primary Question
MHE. OLIVER D. SEMUGURUKA aliuliza:-
Je, lini Serikali itajenga mnara wa simu katika Kata ya Kerebe Muleba?
Name
Maryprisca Winfred Mahundi
Sex
Female
Party
CCM
Constituent
Special Seats
Answer
NAIBU WAZIRI WA MAWASILIANO NA TEKNOLOJIA YA HABARI alijibu:-
Mheshimiwa Spika, Serikali kupitia Mfuko wa Mawasiliano kwa Wote (UCSAF) inaendelea na utekelezaji wa Mradi wa Tanzania ya Kidigitali wa Awamu ya Kwanza (DTP) ambapo mkataba wake ulisainiwa tarehe 13 Mei, 2023 na utekelezaji unatarajiwa kukamilika ifikapo tarehe 12 Mei, 2025. Kupitia mradi huu Kata ya Kerebe imejumuishwa na kupata mtoa huduma wa Vodacom.
Mheshimiwa Spika, utekelezaji wa mradi wa ujenzi wa mnara huu wa Vodacom katika Kata ya Kerebe upo katika hatua za awali ambapo mtoa huduma ameanza uchimbaji wa msingi na ujenzi wa mnara huu. Aidha mnara huu unatarajiwa kukamilika mwishoni mwa mwezi Februari 2025. Hivyo, kukamilika kwa mradi huu kutaboresha huduma za mawasiliano ya simu katika kata hiyo, ambapo mnara huu umelenga kunufaisha Kijiji cha Makibwa na vijiji vingine vya jirani.
Copyright © Bunge Polis 2025. All Rights Reserved