Bunge la Tanzania
Jamhuri ya Muungano ya Tanzania
Term | Session | Sitting | Sector | Ministry | Qn No | Date |
---|---|---|---|---|---|---|
2020-2025 | Session 18 | Sitting 1 | Water and Irrigation | Wizara ya Maji | 12 | 2025-01-28 |
Name
Aida Joseph Khenani
Sex
Female
Party
CHADEMA
Constituent
Nkasi Kaskazini
Primary Question
MHE. AIDA J. KHENANI aliuliza:-
Je, Mradi wa Kutoa Maji Ziwa Tanganyika ili kumaliza changamoto ya maji Nkasi umefikia wapi?
Name
Kundo Andrea Mathew
Sex
Male
Party
CCM
Constituent
Bariadi
Answer
NAIBU WAZIRI WA MAJI alijibu:-
Mheshimiwa Spika, Serikali inatekeleza mkakati wa kutoa maji Ziwa Tanganyika kwa ajili ya kutatua changamoto ya maji katika Mikoa ya Kigoma, Katavi na Rukwa ikiwemo Wilaya ya Nkasi. Serikali kwa sasa ipo katika hatua za mwisho za kumpata mtaalam mshauri kwa ajili ya kufanya usanifu wa kina wa mradi huo ambapo unatarajiwa kuanza mwezi Aprili, 2025.
Copyright © Bunge Polis 2025. All Rights Reserved