Bunge la Tanzania
Jamhuri ya Muungano ya Tanzania
Term | Session | Sitting | Sector | Ministry | Qn No | Date |
---|---|---|---|---|---|---|
2020-2025 | Session 18 | Sitting 1 | Finance and Planning | Wizara ya Fedha | 18 | 2025-01-28 |
Name
Bernadeta Kasabago Mushashu
Sex
Female
Party
CCM
Constituent
Special Seats
Primary Question
MHE. BERNADETA K. MUSHASHU aliuliza:-
Je, lini Serikali itawalipa wateja walioweka fedha zao katika Kagera Cooperative Bank?
Name
Hamad Hassan Chande
Sex
Male
Party
CCM
Constituent
Kojani
Answer
NAIBU WAZIRI WA FEDHA alijibu:-
Mheshimiwa Spika, Januari 4, 2018, Benki Kuu ya Tanzania iliifutia leseni ya biashara benki ya wakulima Mkoa wa Kagera na kuiteua Bodi ya Bima ya Amana kuwa mfilisi wa benki hiyo. Hadi Desemba 2024, jumla ya shilingi milioni 846.16 kati ya shilingi milioni 899.56 sawa na 94.06% zilimelipwa kama fidia ya bima ya amana kwa wateja 1,391 waliojitokeza kati ya wateja 2,797 waliokuwa na amana isiyozidi shilingi 1,500,000. Aidha, katika kipindi hicho, Bodi ya Amana imelipa wadai wa benki fidia ya ufilisi shilingi milioni 664.25 kati ya madai ya shilingi bilioni 1.64 sawa na 40.50% kwa wateja 195 kati ya wateja 274 wanaostahiki kulipwa fidia hiyo.
Mheshimiwa Spika, ninatoa rai kwa Mheshimiwa Mbunge, tuendelee kuhamasisha wananchi wanaodai fedha zao kuwasiliana na Bodi ya Bima ya Amana ili kulipwa stahiki zao.
Mheshimiwa Spika, ahsante.
Copyright © Bunge Polis 2025. All Rights Reserved