Bunge la Tanzania
Jamhuri ya Muungano ya Tanzania
Term | Session | Sitting | Sector | Ministry | Qn No | Date |
---|---|---|---|---|---|---|
2020-2025 | Session 18 | Sitting 1 | Livestock , Fisheries, Agriculture, Food Security and Cooperatives | Wizara ya Mifugo | 19 | 2025-01-28 |
Name
Kilumbe Shabani Ng'enda
Sex
Male
Party
CCM
Constituent
Kigoma Mjini
Primary Question
MHE. KILUMBE S. NG’ENDA aliuliza:-
Je, lini Serikali itakamilisha maboresho ya Kanuni za Uvuvi ili kupata ufumbuzi wa aina ya wavu wa kuvulia samaki aina ya migebuka?
Name
Dr. Ashatu Kachwamba Kijaji
Sex
Female
Party
CCM
Constituent
Kondoa
Answer
NAIBU WAZIRI WA ARDHI, NYUMBA NA MAENDELEO YA MAKAZI K.n.y. WAZIRI WA MIFUGO NA UVUVI alijibu:-
Mheshimiwa Spika, Wizara imekuwa ikifanya maboresho katika Kanuni za Uvuvi za mwaka 2009. Aidha, Kanuni hizi zimekuwa zikiboreshwa kila mara ambapo mwaka 2018, 2019, 2020 na 2022 maboresho yalifanyika ili kukidhi mahitaji ya usimamizi na uendeshaji wa shughuli za uvuvi nchini. Hata hivyo, Wizara imekamilisha utaratibu wa kutoa Waraka wa Matumizi ya Wavu wa Makila kwa ajili ya uvuvi wa samaki aina ya migebuka katika Ziwa Tanganyika ambapo, Waraka huu utakuwa ni hatua za haraka na za awali katika kutatua changamoto inayowakabili wavuvi katika Ziwa Tanganyika.
Copyright © Bunge Polis 2025. All Rights Reserved