Bunge la Tanzania
Jamhuri ya Muungano ya Tanzania
Term | Session | Sitting | Sector | Ministry | Qn No | Date |
---|---|---|---|---|---|---|
2020-2025 | Session 18 | Sitting 1 | Home Affairs | Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi | 6 | 2025-01-28 |
Name
Jafari Chege Wambura
Sex
Male
Party
CCM
Constituent
Rorya
Primary Question
MHE. JAFARI W. CHEGE aliuliza:-
Je, lini wizi wa mifugo utadhibitiwa Wilayani Rorya?
Name
Daniel Baran Sillo
Sex
Male
Party
CCM
Constituent
Babati Vijijini
Answer
NAIBU WAZIRI WA MAMBO YA NDANI YA NCHI alijibu:-
Mheshimiwa Spika, Jeshi la Polisi lina wajibu wa kudhibiti wizi wa mifugo katika Wilaya ya Rorya. Jitihada zinazofanywa na Jeshi la Polisi ni pamoja na kutoa elimu juu ya ulinzi jirani, kuanzisha vikundi vya ulinzi shirikishi na mazizi salama. kuimarisha kikosi cha kupambana na wizi wa mifugo kwa kuongeza askari na vitendea kazi, kufanya mikutano ya ujirani mwema na Polisi Wilaya ya Nyatike ya Nchini Kenya juu ya udhibiti wa makosa yanayovuka mipaka na jitihada zote hizi ni endelevu na zimepunguza kwa kiasi kikubwa wizi wa mifugo. Aidha, takwimu zinaonesha katika kipindi cha mwezi Disemba, 2023 na mwezi Januari, 2024 kumeripotiwa matukio 26 na kipindi kama hicho mwezi Disemba, 2024 na mwezi Januari, 2025 kumeripotiwa matukio tisa, sawa na upungufu wa matukio 17. Ahsante.
Copyright © Bunge Polis 2025. All Rights Reserved