Bunge la Tanzania
Jamhuri ya Muungano ya Tanzania
Term | Session | Sitting | Sector | Ministry | Qn No | Date |
---|---|---|---|---|---|---|
2020-2025 | Session 18 | Sitting 6 | Youth, Disabled, Labor and Employment | Ofisi ya Waziri Mkuu, Kazi, Ajira, Vijana na Wenye Ulemavu | 91 | 2025-02-04 |
Name
Fakharia Shomar Khamis
Sex
Female
Party
CCM
Constituent
Special Seats
Primary Question
MHE. FAKHARIA SHOMAR KHAMIS aliuliza: -
Je, Mstaafu aliyecheleweshewa kupata mafao, anaweza kudai fedha kutokana na usumbufu alioupata wakati anasubiri mafao yake?
Name
Paschal Katambi Patrobas
Sex
Male
Party
CCM
Constituent
Shinyanga Mjini
Answer
NAIBU WAZIRI, OFISI YA WAZIRI MKUU, KAZI, AJIRA, VIJANA NA WENYE ULEMAVU (MHE. PASCHAL P. KATAMBI) alijibu: -
Mheshimiwa Naibu Spika, kwa niaba ya Mheshimiwa Waziri Mkuu naomba kujibu swali la Mheshimiwa Fakharia Shomar Khamis, Mbunge wa Viti Maalum, kama ifuatavyo: -
Mheshimiwa Naibu Spika, Sheria za Mifuko ya Hifadhi ya Jamii ya NSSF na PSSSF katika vifungu 49(3) na 43(3) mtawalia, vinaeleza kuwa endapo mfuko utachelewesha kulipa mafao kwa mwanachama na uchelewesho huo haukusababishwa na mwanachama mwenyewe au mwajiri, Mfuko utamlipa mwanachama huyo mafao yake pamoja na riba ya 15% kwa mwaka, ya kiasi atakachokuwa amelipwa kama mafao kwa Mfuko wa NSSF na asilimia tano kwa Mfuko wa PSSSF.
Mheshimiwa Naibu Spika, hivyo, sheria imetoa haki ya mwanachama kulipwa fidia endapo atacheleweshewa kulipwa mafao yake ikiwa ucheleweshaji huo umesababishwa na mfuko, ahsante.
Copyright © Bunge Polis 2025. All Rights Reserved