Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 18 Sitting 6 Regional Administration and Local Government Authorities Ofisi ya Rais TAMISEMI. 92 2025-02-04

Name

Antipas Zeno Mngungusi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Malinyi

Primary Question

MHE. ALEKSIA A. KAMGUNA K.n.y. MHE. ANTIPAS Z. MGUNGUSI aliuliza: -

Je, lini Serikali itatoa fedha za kukamilisha miradi ya Hospitali ya Wilaya ya Malinyi na Kituo cha Afya cha Ngoheranga?

Name

Dr. Festo John Dugange

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Wanging'ombe

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DKT. FESTO J. DUGANGE) alijibu: -

Mheshimiwa Naibu Spika, mradi wa ujenzi wa Hospitali ya Wilaya ya Malinyi ulianza kutekelezwa katika mwaka wa fedha 2018/2019 ambapo hadi sasa jumla ya shilingi bilioni 3.6 zimetolewa na kuwezesha ujenzi wa majengo 15, ambayo yamekamilika na yanatoa huduma mbalimbali ngazi ya hospitali.

Mheshimiwa Naibu Spika, katika mwaka wa fedha 2019/2020 Serikali ilitoa shilingi milioni 570 kwa ajili ya ujenzi wa Kituo cha Afya Ngoheranga ambapo jumla ya majengo matano, ujenzi umekamilika na kituo kimeanza kutoa huduma.

Mheshimiwa Naibu Spika, Serikali itaendelea kutenga bajeti kwa awamu kwa ajili ya ujenzi wa miundombinu iliyosalia katika Hospitali ya Wilaya pamoja na Kituo cha Afya cha Ngoheranga, ahsante.