Bunge la Tanzania
Jamhuri ya Muungano ya Tanzania
Term | Session | Sitting | Sector | Ministry | Qn No | Date |
---|---|---|---|---|---|---|
2020-2025 | Session 18 | Sitting 6 | Energy and Minerals | Wizara ya Nishati | 95 | 2025-02-04 |
Name
Omari Mohamed Kigua
Sex
Male
Party
CCM
Constituent
Kilindi
Primary Question
MHE. OMAR M. KIGUA aliuliza:-
Je, upi mpango mkakati wa kufikisha nishati ya umeme kwenye maeneo yote ya uchimbaji wa Madini – Kilindi?
Name
Judith Salvio Kapinga
Sex
Female
Party
CCM
Constituent
Special Seats
Answer
NAIBU WAZIRI WA NISHATI alijibu:-
Mheshimiwa Naibu Spika, Wilaya ya Kilindi ina maeneo yapatayo 12 ya uchimbaji wa madini ya dhahabu ambapo kati ya hayo, maeneo manne tayari yameshapatiwa huduma ya umeme. Maeneo hayo ni Mafulila, Mfyalime/Najim, Masagulu Muheza na Chanungu.
Mheshimiwa Naibu Spika, aidha, eneo la Matanda, mkandarasi aitwaye DIEYNEM Company Ltd anaendelea na kazi ya kuweka miundombinu ya umeme na anatarajia kukamilisha kazi hiyo hivi karibuni. Maeneo mengine yaliyosalia yatapata umeme kupitia miradi mbalimbali itakayofuata, ahsante.
Copyright © Bunge Polis 2025. All Rights Reserved