Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2015-2020 Session 2 Sitting 6 Youth, Disabled, Labor and Employment Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi 69 2016-02-02

Name

Kiswaga Boniventura Destery

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Magu

Primary Question

MHE. KISWAGA B. DESTERY aliuliza:-
Pamoja na kwamba polisi ni walinzi wa raia na mali zao, ila wanakabiliwa na changamoto za nyumba za kuishi, maslahi duni na ukosefu wa vitendea kazi:-
(a) Je, Serikali ina mpango gani wa kuboresha vitendea kazi kama magari na mafuta?
(b) Je, Serikali ina mpango gani wa kujenga nyumba za askari polisi na kuboresha mishahara yao?

Name

Eng. Hamad Yussuf Masauni

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kikwajuni

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAMBO YA NDANI alijibu:-
Mheshimiwa Naibu Spika, napenda kujibu swali la Mheshimiwa Kiswaga Boniventura Destery, Mbunge wa Magu lenye sehemu (a) na (b) kama ifuatavyo:-
Mheshimiwa Naibu Spika, Serikali imekuwa ikiboresha hali ya vitendea kazi kwa Jeshi la Polisi ikiwemo vyombo vya usafiri, mawasiliano na zana nyingine za kazi. Mathalani kwa mwaka wa fedha 2015/2016, Serikali ililipatia Jeshi la Polisi jumla ya magari 387 kati ya magari 777 yanayotarajiwa kununuliwa. Aidha, Serikali inatarajia kuongeza fedha ya mafuta na vilainishi katika bajeti ya mwaka wa fedha ya 2016/2017. Ni kweli kuwa Jeshi la Polisi, linakabiliwa na changamoto ya uhaba wa nyumba za makazi ya Askari. Kupitia Mpango Shirikishi wa wadau mbalimbali na mikopo yenye riba nafuu, Serikali inakusudia kujenga nyumba jumla yake ni kama 4,136 katika mikoa 15 pamoja na Mikoa mitano ya Zanzibar.
Mheshimiwa Naibu Spika, vilevile katika kulipatia ufumbuzi wa kudumu tatizo la makazi kwa askari. Serikali inaandaa mpango mkakati wa kujenga nyumba zaidi ya 35,000 kufikia mwaka 2025, ikiwa ni wastani wa takriban nyumba 3,500 wa kila mwaka.
Aidha, Serikali itaendelea kuliwezesha Jeshi la Polisi kutatua changamoto za makazi ya askari kwa kudhamini mikopo nafuu kutoka Taasisi ya kifedha na kuchangia ujenzi wa nyumba pale bajeti inaporuhusu. Kama ilivyo kwa watumishi wengine wa Umma, Serikali imekuwa ikiongeza viwango vya mishahara, kwa Askari wa Jeshi la Polisi kila mwaka.