Bunge la Tanzania
Jamhuri ya Muungano ya Tanzania
Term | Session | Sitting | Sector | Ministry | Qn No | Date |
---|---|---|---|---|---|---|
2020-2025 | Session 18 | Sitting 6 | Livestock , Fisheries, Agriculture, Food Security and Cooperatives | Wizara ya Kilimo | 98 | 2025-02-04 |
Name
Nashon William Bidyanguze
Sex
Male
Party
CCM
Constituent
Kigoma Kusini
Primary Question
MHE. NASHON W. BIDYANGUZE aliuliza: -
Je, miradi mingapi ya umwagiliaji imepangwa kujengwa Wilayani Uvinza kwa mwaka wa fedha 2023/2024?
Name
David Ernest Silinde
Sex
Male
Party
CCM
Constituent
Tunduma
Answer
NAIBU WAZIRI WA KILIMO alijibu: -
Mheshimiwa Naibu Spika, kwa mwaka wa fedha 2023/2024 Wilaya ya Uvinza ilikuwa na miradi minne ya upembuzi yakinifu na usanifu wa kina katika Skimu za Kashagulu, Mgambazi, Nkonkwa na Ilagala. Aidha, hatua za manunuzi kwa ajili ya kumpata mshauri elekezi wa kukamilisha upembuzi yakinifu na usanifu zimekamilika na kazi za upembuzi yakinifu zitaanza mara baada ya hatua za kimkataba kukamilika, ahsante sana. (Makofi)
Copyright © Bunge Polis 2025. All Rights Reserved