Bunge la Tanzania
Jamhuri ya Muungano ya Tanzania
Term | Session | Sitting | Sector | Ministry | Qn No | Date |
---|---|---|---|---|---|---|
2020-2025 | Session 18 | Sitting 6 | Works and Transport | Wizara ya Ujenzi | 99 | 2025-02-04 |
Name
Shabani Omari Shekilindi
Sex
Male
Party
CCM
Constituent
Lushoto
Primary Question
MHE. SHABANI O. SHEKILINDI aliuliza: -
Je, Serikali ina mpango gani wa kumalizia ujenzi wa Barabara ya Mkuzi hadi Mlola Lushoto kwa mkupuo mmoja kwa kiwango cha lami?
Name
Eng. Godfrey Msongwe Kasekenya
Sex
Male
Party
CCM
Constituent
Ileje
Answer
NAIBU WAZIRI WA UJENZI alijibu: -
Mheshimiwa Naibu Spika, ujenzi kwa kiwango cha lami wa barabara ya Magamba – Mkuzi hadi Mlola (kilometa 35.37) unatekelezwa kwa awamu kulingana na upatikanaji wa fedha. Hadi sasa jumla ya kilometa 5.33 kuanzia Magamba hadi Mkuzi zimejengwa kwa kiwango cha lami. Kwa sehemu iliyobaki ya kutoka Mkuzi hadi Mlola (kilometa 30.04), Serikali itaendelea kuijenga kwa kadiri ya fedha zinavyopatikana, ahsante. (Makofi)
Copyright © Bunge Polis 2025. All Rights Reserved