Bunge la Tanzania
Jamhuri ya Muungano ya Tanzania
Term | Session | Sitting | Sector | Ministry | Qn No | Date |
---|---|---|---|---|---|---|
2020-2025 | Session 18 | Sitting 6 | Home Affairs | Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi | 102 | 2025-02-04 |
Name
Omar Issa Kombo
Sex
Male
Party
CCM
Constituent
Wingwi
Primary Question
MHE. OMAR ISSA KOMBO aliuliza: -
Je, lini Serikali itajenga Nyumba za Polisi kwenye Kituo cha Polisi Micheweni?
Name
Daniel Baran Sillo
Sex
Male
Party
CCM
Constituent
Babati Vijijini
Answer
NAIBU WAZIRI WA MAMBO YA NDANI YA NCHI alijibu: -
Mheshimiwa Naibu Spika, Serikali inatarajia kutenga fedha kiasi cha shilingi 368,770,600/= toka kwenye Bajeti ya Serikali ya mwaka wa fedha 2025/2026, kwa ajili ya kujenga nyumba mbili za makazi ya kuishi familia sita za Askari Polisi katika Kituo cha Polisi Micheweni.
Mheshimiwa Naibu Spika, kwa sasa Serikali imetenga fedha kiasi cha shilingi 802,926,788/= kwa ajili ya kujenga kituo kipya cha Polisi daraja “B” cha Micheweni, kwani kituo kilichopo sasa ni kichakavu na hakiwezi kufanyiwa ukarabati. Ujenzi huo unatarajia kuanza katika mwaka wa fedha 2024/2025, ahsante.
Copyright © Bunge Polis 2025. All Rights Reserved