Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Omar Issa Kombo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Wingwi

Primary Question

MHE. OMAR ISSA KOMBO aliuliza: - Je, lini Serikali itajenga Nyumba za Polisi kwenye Kituo cha Polisi Micheweni?

Supplementary Question 1

MHE. OMAR ISSA KOMBO: Mheshimiwa Naibu Spika, nashukuru kwa majibu ya Serikali, lakini kwa kuwa ni muda mrefu nimeuliza maswali kuhusu ujenzi wa Kituo cha Polisi pamoja na nyumba za Askari, na Mheshimiwa Waziri ametuambia kwamba, ametenga shilingi 800,000,000/=, sasa je, ni quarter gani ya mwaka wa fedha ujenzi huu wa Kituo cha Polisi Micheweni utaanza?

Mheshimiwa Naibu Spika, swali la pili. Je, Mheshimiwa Naibu Waziri uko tayari kupanga ratiba yako baada ya Mkutano huu wa Bunge, kuambatana nami kwenda kutembelea Kituo hiki cha Polisi Micheweni?

Name

Daniel Baran Sillo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Babati Vijijini

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAMBO YA NJE YA NCHI: Mheshimiwa Naibu Spika, kama nilivyosema, fedha imetengwa kwenye mwaka wa fedha 2024. Kwa hiyo, kwenye quarter hii ya tatu na ya nne itatolewa kwa ajili ya ujenzi wa kituo hicho cha Polisi.

Mheshimiwa Naibu Spika, kuhusu utayari wa Kwenda huko baada ya Bunge lako Tukufu; nitakaa na Mheshimiwa Mbunge, tutapanga ratiba ya kwenda kutembelea Kituo hicho cha Micheweni, ahsante.

Name

Kunti Yusuph Majala

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. OMAR ISSA KOMBO aliuliza: - Je, lini Serikali itajenga Nyumba za Polisi kwenye Kituo cha Polisi Micheweni?

Supplementary Question 2

MHE. KUNTI Y. MAJALA: Mheshimiwa Naibu Spika, naomba kumwuliza swali Mheshimiwa Naibu Waziri. Tuliomba fedha za ukarabati wa Vituo vya Polisi Kwamtoro pamoja na Mrijo na tuliahidiwa mwaka huu wa fedha wangetoa hiyo fedha, lakini mpaka sasa fedha haijaenda. Ni lini Serikali itapeleka fedha kwa ajili ya ukarabati wa vituo viwili vya Polisi; Kwamtoro pamoja na Mrijo, Wilayani Chemba?

Name

Daniel Baran Sillo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Babati Vijijini

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAMBO YA NJE YA NCHI: Mheshimiwa Naibu Spika, kama tulivyosema katika mwaka wa fedha 2024/2025 tutapeleka fedha, kwa kuwa mwaka bado unaendelea. Kwa hiyo, Mheshimiwa Mbunge asiwe na wasiwasi fedha itakuja kwa ajili ya ukarabati wa vituo viwili vya Polisi vya Chemba, ahsante.

Name

Boniphace Mwita Getere

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Bunda

Primary Question

MHE. OMAR ISSA KOMBO aliuliza: - Je, lini Serikali itajenga Nyumba za Polisi kwenye Kituo cha Polisi Micheweni?

Supplementary Question 3

MHE. BONIPHACE M. GETERE: Mheshimiwa Naibu Spika, nakushukuru. Kituo cha Polisi cha Mgeta, Serikali imetoa shilingi 53,000,000/= na sasa ghafla kimesimama, hakiendelei kujengwa. Ni lini sasa kituo hicho kitamalizika?

Name

Daniel Baran Sillo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Babati Vijijini

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAMBO YA NJE YA NCHI: Mheshimiwa Naibu Spika, kama ambavyo tumeshatoa fedha kiasi cha shilingi 53,000,000/=, basi namhakikishia Mheshimiwa Mbunge, baada ya kipindi cha maswali, nitakutananaye. Tutafuatilia ni kwa nini kituo hicho kisikamilike wakati fedha imetolewa? Ahsante