Bunge la Tanzania
Jamhuri ya Muungano ya Tanzania
Term | Session | Sitting | Sector | Ministry | Qn No | Date |
---|---|---|---|---|---|---|
2020-2025 | Session 18 | Sitting 6 | Regional Administration and Local Government Authorities | Ofisi ya Rais TAMISEMI. | 130 | 2025-02-06 |
Name
Samweli Xaday Hhayuma
Sex
Male
Party
CCM
Constituent
Hanang'
Primary Question
MHE. SAMWELI X. HHAYUMA aliuliza:-
Je, nini mkakati wa Serikali wa kuboresha zahanati za zamani zilizopo Makao Makuu ya Kata za Hanang’?
Name
Dr. Festo John Dugange
Sex
Male
Party
CCM
Constituent
Wanging'ombe
Answer
NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DKT. FESTO J. DUGANGE) alijibu:-
Mheshimiwa Spika, Serikali inatambua uwepo wa vituo vya huduma ambavyo ni vikongwe na chakavu vinavyohitaji ukarabati. Ili kutekeleza jukumu hilo, Serikali ilifanya tathmini ya vituo chakavu, ambapo mpaka Disemba, 2024 kuna jumla ya vituo vya afya 204 na zahanati 1,226 zinazohitaji ukarabati kote nchini zikiwemo Zahanati za Sirop, Getanuwas na Dirma katika Wilaya ya Hanang’
Mheshimiwa Spika, Serikali inaendelea na ukarabati wa vituo chakavu kwa awamu na mpango wa Serikali ni kuongeza kasi ya ukarabati wa vituo vya afya na zahanati mara baada ya kukamilisha ukarabati wa hospitali kongwe 77 ambapo tayari hospitali 14 zimekwisha karabatiwa na hospitali 34 ukarabati unaendelea ambapo jumla ya shilingi shilingi bilioni 44.5. Ahsante.
Copyright © Bunge Polis 2025. All Rights Reserved