Bunge la Tanzania
Jamhuri ya Muungano ya Tanzania
Term | Session | Sitting | Sector | Ministry | Qn No | Date |
---|---|---|---|---|---|---|
2020-2025 | Session 18 | Sitting 8 | Regional Administration and Local Government Authorities | Ofisi ya Rais TAMISEMI. | 131 | 2025-02-06 |
Name
Felista Deogratius Njau
Sex
Female
Party
CHADEMA
Constituent
Special Seats
Primary Question
MHE. FELISTA D. NJAU aliuliza:-
Je, lini Serikali itajenga shule mpya ya sekondari katika Kata ya Mabogini, Moshi Vijijini?
Name
Dr. Festo John Dugange
Sex
Male
Party
CCM
Constituent
Wanging'ombe
Answer
NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA – (MHE. FESTO J. DUGANGE) alijibu:-
Mheshimiwa Spika, Kata ya Mabogini ina jumla ya shule za sekondari tatu ambazo ni Mpirani yenye jumla ya wanafunzi 1,158, Mabogini wanafunzi 711 na Mtakuja B wanafunzi 234. Aidha, Mwaka wa Fedha 2022/2023 Serikali ilipeleka shilingi milioni 584.2, kwa ajili ya ujenzi wa shule ya kutwa katika Kata ya Mabogini. Ujenzi wa shule hii umekamilika na kusajiliwa kwa jina la Mtakuja B Sekondari.
Mheshimiwa Spika, mpango wa Serikali kwa sasa ni kujenga shule za kutwa kwa kuzingatia vigezo vitatu ambavyo ni, kila kata kuwa na shule ya sekondari walau moja katika maeneo ya msongamono mkubwa wa wanafunzi na sehemu ambazo watoto wanatembea zaidi ya kilometa 5. Kwa kuzingatia kuwa, Kata ya Mabogini tayari ina shule tatu za sekondari, haijaingizwa kwenye mpango wa kujengewa shule nyingine ya sekondari. Ahsante.
Copyright © Bunge Polis 2025. All Rights Reserved