Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2015-2020 Session 4 Sitting 5 Home Affairs Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi 67 2016-09-13

Name

Hasna Sudi Katunda Mwilima

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Kigoma Kusini

Primary Question

MHE. HASNA S. K. MWILIMA aliuliza:-
Gereza la Ilagala limehodhi eneo kubwa la shamba na kufanya wananchi wa Kata ya Ilagala kukosa maeneo ya kulima.
Je, Serikali haioni umuhimu wa kutoa sehemu ya eneo kwa ajili ya wananchi wa Ilagala ili na wao waweze kupata maeneo ya kulima?

Name

Dr. Mwigulu Lameck Nchemba Madelu

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Iramba Magharibi

Answer

WAZIRI WA MAMBO YA NDANI YA NCHI alijibu:-
Mheshimiwa Naibu Spika, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Hasna Sudi Katunda Mwilima, Mbunge wa Kigoma Kusini, kama ifuatavyo:-
Mheshimiwa Naibu Spika, Gereza la Ilagala ni gereza la kilimo na mifugo ambapo linamiliki jumla ya ekari 10,760 na kati ya ekari hizo, ekari 4,500 ziko katika milima na mabonde ambapo zimehifadhiwa kwani ni vyanzo vya mito katika eneo hilo. Ekari 3,000 zimetengwa na zinatumika kwa ajili ya ufugaji wa ng‟ombe, mbuzi na kondoo; na ekari 5,000 kwa ajili ya makazi na ekari 2,760 ni kwa ajili ya kilimo cha mazao ya mahindi; mahindi ya mbegu, michikichi, mihogo, mbaazi, mboga pamoja na matunda. Hata hivyo, pamoja na shughuli tajwa hapo juu, eneo hilo bado halitoshelezi kwa ajili ya mahitaji yaliyokusudiwa.