Bunge la Tanzania
Jamhuri ya Muungano ya Tanzania
Term | Session | Sitting | Sector | Ministry | Qn No | Date |
---|---|---|---|---|---|---|
2020-2025 | Session 18 | Sitting 12 | Works and Transport | Wizara ya Uchukuzi | 210 | 2025-02-12 |
Name
Stella Ikupa Alex
Sex
Female
Party
CCM
Constituent
Special Seats
Primary Question
MHE. STELLA I. ALEX aliuliza:-
Je, nini mkakati wa Serikali kuhakikisha miundombinu na mazingira ya usafiri kwa watu wenye ulemavu inakuwa rafiki katika treni ya SGR?
Name
Prof. Makame Mnyaa Mbarawa
Sex
Male
Party
CCM
Constituent
Mkoani
Answer
NAIBU WAZIRI WA UJENZI K.n.y. WAZIRI WA UCHUKUZI alijibu:-
Mheshimiwa Naibu Spika, ujenzi wa miundombinu ya reli pamoja na majengo umezingatia uwepo wa miundombinu wezeshi kwa watu wenye mahitaji maalumu ikiwa ni pamoja na uwekaji wa alama maalum zinazowasaidia kuwaongoza ndani ya majengo pamoja na huduma ya maliwato kwa kuweka vyoo maalum. Vilevile, katika mabehewa tumezingatia uwepo wa sehemu maalum kwa ajili ya kuwawezesha watu wenye mahitaji maalum kuweka viti vyao (wheel chair) pamoja na uwepo wa nukta nundu kuwasaidia kuona.
Mheshimiwa Naibu Spika, aidha, Shirika la Reli limenunua na litaendelea kununua na kuweka viti maalum (wheel chairs) katika majengo ya stesheni kwa lengo la watu wenye mahitaji maalum kutopata changamoto za utumiaji wa huduma za treni. Ahsante.
Copyright © Bunge Polis 2025. All Rights Reserved