Bunge la Tanzania
Jamhuri ya Muungano ya Tanzania
Term | Session | Sitting | Sector | Ministry | Qn No | Date |
---|---|---|---|---|---|---|
2020-2025 | Session 18 | Sitting 12 | Industries and Trade | Wizara ya Viwanda na Biashara | 211 | 2025-02-12 |
Name
Selemani Jumanne Zedi
Sex
Male
Party
CCM
Constituent
Bukene
Primary Question
MHE. SELEMANI J. ZEDI aliuliza:-
Je, kuna mpango gani wa kutoa mafunzo ya utaalam, mitaji, kuwaunganisha na masoko wajasiriamali wanaoongeza thamani ya mazao?
Name
Exaud Silaoneka Kigahe
Sex
Male
Party
CCM
Constituent
Mufindi Kaskazini
Answer
NAIBU WAZIRI WA VIWANDA NA BIASHARA alijibu:-
Mheshimiwa Naibu Spika, Serikali kupitia Shirika la Maendeleo ya Viwanda Vidogo Tanzania (SIDO) inaendelea na utekelezaji wa mpango wake wa kuwawezesha wajasiriamali katika shughuli zao ikiwa ni pamoja na uongezaji thamani mazao.
Mheshimiwa Naibu Spika, utekelezaji huo hufanywa kwa kutoa mafunzo, ushauri, uwezeshaji upatikanaji wa teknolojia za usindikaji wa mazao ya kilimo na uchakataji wa bidhaa mbalimbali, kuwawezesha Wajasiriamali kupata mitaji ambapo SIDO imekuwa ikitoa mikopo midogo pamoja na kuwaunganisha wajasiriamali wenye mahitaji ya mikopo mikubwa na Taasisi za kifedha ambazo Shirika limeingia nazo makubaliano.
Mheshimiwa Naibu Spika, kuwaunganisha pia wajasiriamali kushiriki katika maonesho yanayoandaliwa na wadau mbalimbali kitaifa na kimataifa kwa lengo la kutangaza bidhaa na kupata soko la bidhaa zao. Ninakushukuru.
Copyright © Bunge Polis 2025. All Rights Reserved