Bunge la Tanzania
Jamhuri ya Muungano ya Tanzania
Term | Session | Sitting | Sector | Ministry | Qn No | Date |
---|---|---|---|---|---|---|
2020-2025 | Session 18 | Sitting 12 | Industries and Trade | Wizara ya Viwanda na Biashara | 212 | 2025-02-12 |
Name
Janeth Elias Mahawanga
Sex
Female
Party
CCM
Constituent
Special Seats
Primary Question
MHE. JANETH E. MAHAWANGA aliuliza:-
Je, lini TBS itaweka utaratibu wa kutoa elimu kwa Wajasiriamali wadogo wanaojihusisha na biashara ya kusindika vyakula?
Name
Exaud Silaoneka Kigahe
Sex
Male
Party
CCM
Constituent
Mufindi Kaskazini
Answer
NAIBU WAZIRI WA VIWANDA NA BIASHARA alijibu:-
Mheshimiwa Naibu Spika, Serikali kwa kupitia Shirika la Viwango Tanzania (TBS), imekuwa na utaratibu wa kutoa mafunzo kwa Wajasiriamali wadogo na wa kati wanaojihusisha na biashara ya kusindika bidhaa mbalimbali ikiwemo bidhaa za vyakula. Mafunzo hayo hutolewa kwa kuzingatia Mpango Mkakati wa Shirika na Mpango Kazi wa Mafunzo kwa Wajasiriamali unaoandaliwa kila mwaka.
Mheshimiwa Naibu Spika, katika utekelezaji wa mpango huo, mafunzo hayo ambayo yamekuwa yakitolewa kwa kushirikiana na SIDO na utaratibu huo umesaidia, si tu kusindika vyakula, bali na kupata teknolojia sahihi zinazosaidia kuzalisha bidhaa zenye viwango, lakini pia kupata mikopo, majengo na elimu ya biashara na masoko. Ninakushukuru sana.
Copyright © Bunge Polis 2025. All Rights Reserved