Bunge la Tanzania
Jamhuri ya Muungano ya Tanzania
Term | Session | Sitting | Sector | Ministry | Qn No | Date |
---|---|---|---|---|---|---|
2020-2025 | Session 18 | Sitting 12 | Education, Science,Technology and Vocational Training, | Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia | 214 | 2025-02-12 |
Name
Shally Josepha Raymond
Sex
Female
Party
CCM
Constituent
Special Seats
Primary Question
MHE. SHALLY J. RAYMOND aliuliza:-
Je, vituo vingapi vya umahiri vya sayansi na teknolojia na Akili Mnemba katika Taasisi za Elimu ya Juu vimeanzishwa?
Name
Omary Juma Kipanga
Sex
Male
Party
CCM
Constituent
Mafia
Answer
NAIBU WAZIRI WA ELIMU, SAYANSI NA TEKNOLOJIA alijibu:-
Mheshimiwa Naibu Spika, Serikali imeanzisha jumla ya vituo vya umahiri 13 kati ya vituo 13, sawa na 100% ya lengo la miaka mitano katika Taasisi za Elimu ya Juu. Lengo la kuanzishwa kwa vituo hivyo ni kuimarisha uwezo katika utoaji wa elimu ya juu na utafiti katika maeneo ya afya na baiolojia ya molekuli; TEHAMA; kilimo na mifugo; maji na nishati jadidifu. Aidha, Serikali itaendelea kuanzisha vituo vipya vya umahiri kulingana na mahitaji, hususan katika kuimarisha mchango wa utafiti na ubunifu katika maendeleo ya kiuchumi na kijamii. Ninakushukuru sana.
Copyright © Bunge Polis 2025. All Rights Reserved