Bunge la Tanzania
Jamhuri ya Muungano ya Tanzania
Term | Session | Sitting | Sector | Ministry | Qn No | Date |
---|---|---|---|---|---|---|
2020-2025 | Session 19 | Sitting 2 | Regional Administration and Local Government Authorities | Ofisi ya Rais TAMISEMI. | 17 | 2025-04-09 |
Name
Juliana Daniel Shonza
Sex
Female
Party
CCM
Constituent
Special Seats
Primary Question
MHE. JULIANA D. SHONZA aliuliza:-
Je, lini Serikali itajenga Kituo cha Afya katika Kata ya Luswisi?
Name
Dr. Festo John Dugange
Sex
Male
Party
CCM
Constituent
Wanging'ombe
Answer
NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DKT. FESTO J. DUGANGE) alijibu:-
Mheshimiwa Naibu Spika, Serikali imeendelea kujenga vituo vya kutolea huduma za afya kwenye Mamlaka za Serikali za Mitaa nchini. Katika kipindi cha kuanzia mwaka wa fedha 2020/2021 hadi 2023/2024 jumla ya vituo vya afya 367 vimejengwa na vinatoa huduma.
Mheshimiwa Naibu Spika, Kata ya Luswisi ipo umbali wa takribani kilometa tano kutoka Kituo cha Afya cha Lubanda na idadi ya wananchi wapatao 4,155 kati ya angalau 10,000 wanaohitajika kwa mujibu wa vigezo.
Mheshimiwa Naibu Spika, Serikali itaendeea kujenga vituo vya afya katika kata za kimkakati kote nchini zikiwemo kata zitakazokidhi vigezo katika Halmashauri ya Wilaya ya Ileje.
Copyright © Bunge Polis 2025. All Rights Reserved