Bunge la Tanzania
Jamhuri ya Muungano ya Tanzania
Term | Session | Sitting | Sector | Ministry | Qn No | Date |
---|---|---|---|---|---|---|
2020-2025 | Session 19 | Sitting 2 | Regional Administration and Local Government Authorities | Ofisi ya Rais TAMISEMI. | 18 | 2025-04-09 |
Name
Dr. Florence George Samizi
Sex
Female
Party
CCM
Constituent
Muhambwe
Primary Question
MHE. KAVEJURU E. FELIX K.n.y. MHE. DKT. FLORENCE G. SAMIZI aliuliza:-
Je, lini Mabweni ya Sekondari ya Busagara na Kumgogo – Muhambwe yatajengwa ili kuanza kidato cha tano na sita?
Name
Zainab Athuman Katimba
Sex
Female
Party
CCM
Constituent
Special Seats
Answer
NAIBU WAZIRI OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. ZAINAB A. KATIMBA) alijibu:-
Mheshimiwa Naibu Spika, mwaka 2023/2024 Serikali ilipeleka shilingi milioni 680 kwa ajili ya ujenzi wa mabweni katika Shule za Sekondari Busagara (mabweni matatu) na Kumgogo (mabweni mawili).
Mheshimiwa Naibu Spika, Shule za Sekondari Busagara na Kumgogo zimeanza kupokea wanafunzi wa kidato cha tano mwaka 2024 ambapo Shule ya Sekondari Busagara ilipangiwa wanafunzi 88 na Shule ya Sekondari Kumgogo ilipangiwa wanafunzi 93.
Mheshimiwa Naibu Spika, Serikali itaendelea kuboresha miundombinu ya shule za sekondari zikiwemo Shule za Busagara na Kumgogo kadri ya upatikanaji wa fedha.
Copyright © Bunge Polis 2025. All Rights Reserved