Bunge la Tanzania
Jamhuri ya Muungano ya Tanzania
Term | Session | Sitting | Sector | Ministry | Qn No | Date |
---|---|---|---|---|---|---|
2020-2025 | Session 19 | Sitting 2 | Finance | Wizara ya Fedha | 23 | 2025-04-09 |
Name
Jacqueline Kandidus Ngonyani (Msongozi)
Sex
Female
Party
CCM
Constituent
Special Seats
Primary Question
MHE. JACQUELINE N. MSONGOZI aliuliza:-
Je, Serikali ina mpango gani wa kupunguza tozo na kodi za uingizaji wa samaki toka nje ya nchi?
Name
Hamad Hassan Chande
Sex
Male
Party
CCM
Constituent
Kojani
Answer
NAIBU WAZIRI WA FEDHA alijibu:-
Mheshimiwa Naibu Spika, Serikali kupitia Kamati ya Maboresho ya Mfumo wa Kodi (Task Force on Tax Reforms) katika vikao vyake, inaendelea kupokea mapendekezo yanayowasilishwa na wadau kuhusu maboresho ya mfumo wa kodi, ada na tozo mbalimbali ikiwa ni pamoja na eneo la uingizaji wa samaki kutoka nje ya nchi.
Mheshimiwa Naibu Spika, tathmini ya kina hufanyika ili kubaini hali ya soko, tabia za walaji, mahitaji, gharama, athari kwa mapato ya Serikali na kuzingatia umuhimu wa kulinda walaji na wafanyabiashara wa ndani ili kuongeza mchango wa thamani katika mnyororo wa uchumi. Hivyo, maamuzi na mapendekezo ya kupunguza tozo na kodi za uingizaji wa samaki kutoka nje ya nchi yatafanywa kulingana na matokeo ya tathmini husika. Ahsante sana.
Copyright © Bunge Polis 2025. All Rights Reserved