Bunge la Tanzania
Jamhuri ya Muungano ya Tanzania
Term | Session | Sitting | Sector | Ministry | Qn No | Date |
---|---|---|---|---|---|---|
2020-2025 | Session 19 | Sitting 2 | Livestock , Fisheries, Agriculture, Food Security and Cooperatives | Wizara ya Kilimo | 25 | 2025-04-09 |
Name
Emmanuel Peter Cherehani
Sex
Male
Party
CCM
Constituent
Ushetu
Primary Question
MHE. EMMANUEL P. CHEREHANI aliuliza:-
Je, lini Serikali itajenga Skimu ya Umwagiliaji katika Jimbo la Ushetu? (Makofi)
Name
David Ernest Silinde
Sex
Male
Party
CCM
Constituent
Tunduma
Answer
NAIBU WAZIRI WA KILIMO alijibu:-
Mheshimiwa Naibu Spika, Jimbo la Ushetu na Halmashauri ya Wilaya ya Ushetu lina mabonde mengi yaliyoainishwa kufaa kwa kilimo cha umwagiiliaji ikiwemo Ulowa, Kisuke, Bulugwa, Butibu, Nimbo, Nyamilangano, Sabasabini, Chona, Chambo, Mpunze, Mwadui na Bugomba B.
Mheshimiwa Naibu Spika, kwa mwaka wa fedha 2024/2025 Serikali kupitia Tume ya Taifa ya Umwagiliaji imeanza kufanya upembuzi yakinifu na usanifu wa kina kwa mabwawa na skimu za umwagiliaji katika Mabonde ya Kisuke, Nimbo na Bulugwa, Butibu kupitia mshauri elekezi ikiwa ni hatua ya kwanza kabla ya kuanza ujenzi. Aidha, kukamilika kwa kazi hii kutasaidia kujua gharama halisi za utekelezaji wa mradi.
Copyright © Bunge Polis 2025. All Rights Reserved