Bunge la Tanzania
Jamhuri ya Muungano ya Tanzania
Term | Session | Sitting | Sector | Ministry | Qn No | Date |
---|---|---|---|---|---|---|
2020-2025 | Session 19 | Sitting 3 | Regional Administration and Local Government Authorities | Ofisi ya Rais TAMISEMI. | 32 | 2025-04-10 |
Name
Amandus Julius Chinguile
Sex
Male
Party
CCM
Constituent
Nachingwea
Primary Question
MHE. JUSTIN L. NYAMOGA K.n.y. MHE. AMANDUS J. CHINGUILE aliuliza:-
Je, ni lini Serikali itaipandisha hadhi Mamlaka ya Mji Mdogo Nachingwea kuwa Mamlaka ya Mji?
Name
Dr. Festo John Dugange
Sex
Male
Party
CCM
Constituent
Wanging'ombe
Answer
NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DKT. FESTO J. DUGANGE) alijibu:-
Mheshimiwa Naibu Spika, uanzishaji wa maeneo ya utawala katika Mamlaka za Serikali za Mitaa hufanyika kwa mujibu wa Sheria za Serikali za Mitaa (Mamlaka za Wilaya), Sura 287, (Mamlaka za Miji), Sura 288 pamoja na Mwongozo wa Uanzishwaji wa Maeneo ya Utawala wa Mwaka 2014. Mwongozo wa kuanzisha maeneo ya utawala unaanza kwa kusudio kujadiliwa kupitia vikao vya ngazi za msingi, Baraza la Madiwani, Kamati ya Ushauri ya Wilaya (DCC) na Kamati ya Ushauri ya Mkoa (RCC). Aidha, Halmashauri ya Wilaya ya Nachingwea inashauriwa kufuata utaratibu huo na kuwasilisha Ofisi ya Rais, TAMISEMI.
Mheshimiwa Naibu Spika, kwa kuwa, mamlaka nyingi zilizoanzishwa bado zina upungufu wa miundombinu mbalimbali yakiwemo majengo ya utawala na huduma za kijamii, kwa sasa Serikali imeweka kipaumbele katika kuboresha miundombinu iliyopo katika maeneo ya utawala yaliyopo. Ahsante.
Copyright © Bunge Polis 2025. All Rights Reserved