Bunge la Tanzania
Jamhuri ya Muungano ya Tanzania
Term | Session | Sitting | Sector | Ministry | Qn No | Date |
---|---|---|---|---|---|---|
2020-2025 | Session 19 | Sitting 3 | Regional Administration and Local Government Authorities | Ofisi ya Rais TAMISEMI. | 33 | 2025-04-10 |
Name
Dr. Medard Matogolo Kalemani
Sex
Male
Party
CCM
Constituent
Chato
Primary Question
MHE. DKT. MEDARD M. KALEMANI aliuliza:-
Je, lini Serikali itakarabati shule kongwe za msingi katika Jimbo la Chato?
Name
Zainab Athuman Katimba
Sex
Female
Party
CCM
Constituent
Special Seats
Answer
NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. ZAINAB A. KATIMBA) alijibu:-
Mheshimiwa Naibu Spika, Mwaka wa Fedha 2024/2025, Serikali imetenga shilingi 476,200,000, kwa ajili ya ujenzi wa madarasa 10 na matundu ya vyoo 77 katika Shule Kongwe za Bwanga, Bwina, Busalala, Ilemela, Itanga, Katale, Katende, Mwangaza, Nyantimba, Nyarutembo na Nyisanzi zilizopo katika Halmashauri ya Wilaya ya Chato. Katika Mwaka wa Fedha 2025/2026, Serikali imepanga kutumia shilingi 890,300,000, kwa ajili ya ujenzi wa madarasa 25 na matundu ya vyoo 75 katika Shule Kongwe za Bukiriguru, Busaka, Buzirayombo, Ihanga, Katete, Kibumba, Kinsabe, Katende, Kitela, Mwabasabi, Minkoto, Mwangaza, Nyakato, Nyamirembe na Nyangh’omango.
Mheshimiwa Naibu Spika, Serikali itaendelea kuboresha shule kongwe za msingi zikiwemo za Halmashauri ya Chato kadri ya upatikanaji wa fedha.
Copyright © Bunge Polis 2025. All Rights Reserved