Bunge la Tanzania
Jamhuri ya Muungano ya Tanzania
Term | Session | Sitting | Sector | Ministry | Qn No | Date |
---|---|---|---|---|---|---|
2020-2025 | Session 19 | Sitting 3 | Energy and Minerals | Wizara ya Nishati | 35 | 2025-04-10 |
Name
Kwagilwa Reuben Nhamanilo
Sex
Male
Party
CCM
Constituent
Handeni Mjini
Primary Question
MHE. RASHID A. SHANGAZI K.n.y. MHE. KWAGILWA R. NHAMANILO aliuliza:-
Je, Serikali ina maelezo gani juu ya kero sugu ya kukatika umeme mara kwa mara Handeni Mjini na ni lini kero hiyo itatatuliwa?
Name
Judith Salvio Kapinga
Sex
Female
Party
CCM
Constituent
Special Seats
Answer
NAIBU WAZIRI WA NISHATI alijibu:-
Mheshimiwa Naibu Spika, changamoto ya kukatika umeme Wilayani Handeni inatokana na uchakavu wa miundombinu ya kusambaza umeme pamoja na urefu wa njia za kusambaza umeme. Katika kukabiliana na changamoto hii, Serikali kupitia TANESCO inaendelea na ukarabati wa miundombinu ya umeme, ikiwa ni pamoja na kubadilisha nguzo za miti na kuweka za zege. Aidha, Serikali kupitia Mradi wa Gridi Imara inaendelea na ujenzi wa Kituo cha Kupoza Umeme cha Mkata, Handeni ambapo kwa sasa mkandarasi yupo kwenye hatua za awali za ujenzi. Aidha, ujenzi wa Kituo cha Kupoza Umeme cha Kilindi umefikia 35% na ujenzi wa njia ya kusafirisha umeme msongo wa kilovoti 132 kutoka Mkata – Handeni hadi Kilindi umefikia 30%. Kukamilika kwa kazi hizi kutawezesha kuondoa kero sugu ya kukatika umeme Handeni Mjini. Ahsante.
Copyright © Bunge Polis 2025. All Rights Reserved