Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2015-2020 Session 4 Sitting 7 Defence and National Service Wizara ya Ulinzi na Jeshi la Kujenga taifa 87 2016-09-15

Name

Julius Kalanga Laizer

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Monduli

Primary Question

MHE. CECILIA D. PARESSO (K.n.y. MHE. JULIUS K. LAIZER) aliuliza:-
Kwa muda mrefu kumekuwa na mgogoro wa mipaka kati ya Jeshi la Wananchi wa Tanzania na Kijiji cha Lashaine Wilayani Monduli, lakini mwaka 2011 yalifikiwa makubaliano chini ya Mkuu wa Wilaya kuwa mipaka yenye mgogoro isomwe upya kwa kutumia GPS na wananchi wa kijiji cha Lashaine wamekuwa wakisubiri zoezi la kusomwa upya mipaka kwa muda mrefu.
Je, Serikali itakamilisha lini makubaliano haya kwa kutumia GPS kusoma mipaka upya ili kumaliza mgogoro huo?

Name

Dr. Hussein Ali Mwinyi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kwahani

Answer

WAZIRI WA ULINZI NA JESHI LA KUJENGA TAIFA alijibu:-
Mheshimiwa Spika, napenda kujibu swali la Mheshimiwa Julius Laizer, Mbunge wa Monduli, kama ifuatavyo:-
Mheshimiwa Spika, vijiji vinavyozunguka eneo la Jeshi la Monduli vimekuwa na migogoro ya mipaka na Jeshi kwa miaka mingi. Katika kumaliza migogoro hiyo, Wizara yangu kwa kushirikiana na Halmashauri ya Wilaya ya Monduli ilifanya vikao na makubaliano ya mipaka eneo la Jeshi na kulipima kwa kutumia vifaa vya kisasa yaani GPS mwaka 2004. Eneo la Jeshi lilipunguzwa kutoka ukubwa wa hekta 94,000 hadi hekta 86,966 ili kupisha makazi ya raia wa vijiji jirani yaliyokuwa yameingilia eneo la Jeshi kikiwemo Kijiji cha Lashaine.
Mheshimiwa Spika, tatizo la mpaka wa Jeshi upande wa Kijiji cha Lashaine ni kuzibainisha beacons zilizowekwa ili wananchi waweze kuziona kwa wazi kwa mujibu wa ramani iliyosajiliwa yaani boundary recovery.
Mheshimiwa Spika, napenda kumhakikishia Mheshimiwa Laizer kuwa azma yetu ya kufufua mpaka huo bado ipo na tutafanya hivyo tutakapopata fedha za kutekeleza jukumu hilo.