Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Cecilia Daniel Paresso

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. CECILIA D. PARESSO (K.n.y. MHE. JULIUS K. LAIZER) aliuliza:- Kwa muda mrefu kumekuwa na mgogoro wa mipaka kati ya Jeshi la Wananchi wa Tanzania na Kijiji cha Lashaine Wilayani Monduli, lakini mwaka 2011 yalifikiwa makubaliano chini ya Mkuu wa Wilaya kuwa mipaka yenye mgogoro isomwe upya kwa kutumia GPS na wananchi wa kijiji cha Lashaine wamekuwa wakisubiri zoezi la kusomwa upya mipaka kwa muda mrefu. Je, Serikali itakamilisha lini makubaliano haya kwa kutumia GPS kusoma mipaka upya ili kumaliza mgogoro huo?

Supplementary Question 1

MHE. CECILIA D. PARESSO: Mheshimiwa Spika, ahsante naomba kuuliza maswali madogo mawili ya nyongeza.
Kwa kuwa makubalinao hayo yalifikiwa mwaka 2011 na sasa ni miaka sita, na tatizo hili limeendelea kuwepo; je, ni lini sasa kwa uhakika kabisa Serikali itaenda kumaliza huu mgogoro uliopo kati ya wananchi na eneo hilo la Jeshi?
Swali la pili, kwa kuwa migogoro hii ya mipaka ya Jeshi na maeneo ya wananchi haipo tu Monduli, iko katika maeneo mbalimbali kwa sababu mimi ni Mjumbe wa Kamati ya Bunge ya Mambo ya Nje, nafahamu kumekuwa na mgogoro huu katika maeneo mengi ambapo Jeshi ina kambi zao. Sasa ni lini kwa uhakika Serikali itatuletea taarifa hapa Bungeni kwamba ina mkakati huu wa kwenda kumaliza matatizo hayo?

Name

Dr. Hussein Ali Mwinyi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kwahani

Answer

WAZIRI WA ULINZI NA JESHI LA KUJENGA TAIFA: Mheshimiwa Spika, ni kweli kwamba mgogoro huu ni wa siku nyingi na kwamba sasa hivi wakati umefika upatiwe ufumbuzi wa kudumu.
Mheshimiwa Spika, nilieleze Bunge lako Tukufu kwamba katika mwaka huu wa fedha, bajeti ya Wizara yangu ilitenga shilingi bilioni 12 kwa ajili ya shughuli za uthamini, upimaji na ulipaji wa fidia katika maeneo mbalimbali. Kwa hiyo, tukianza kupata fedha hizo hususan tatizo dogo kama hili la kuhuisha tu mipaka litashughulikiwa mara moja.
Mheshimiwa Spika, kuhusu swali la pili la kwamba migogoro hii iko mingi na lini taarifa italetwa, nataka nikiri kwamba sehemu nyingi za nchi yetu migogoro baina ya vijiji na Kambi za Jeshi ipo na kama nilivyosema awali tatizo ni fedha za kufanya uthamini kwa yale maeneo ambayo hayajathaminiwa, fedha za kufanya upimaji kwa maeneo yanayohitaji kupimwa na fedha za kulipa fidia kwa maeneo ambayo Jeshi linatakiwa kufidia.
Mheshimiwa Spika, ikumbukwe pia kwamba kuna maeneo mengi ambayo wananchi ndiyo wameingia katika maeneo ya Jeshi. Kwa hiyo, inabidi waelekezwe, waelimishwe wasiwe wanavamia maeneo ya Jeshi. Napenda kuliarifu Bunge lako Tukufu kwamba tutakapoanza tu kupokea hizi fedha, kazi zote hizi nilizozitaja zitaanza kufanywa ili tuondoe migogoro hii inayokabili Jeshi letu na wananchi.

Name

Deo Kasenyenda Sanga

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Makambako

Primary Question

MHE. CECILIA D. PARESSO (K.n.y. MHE. JULIUS K. LAIZER) aliuliza:- Kwa muda mrefu kumekuwa na mgogoro wa mipaka kati ya Jeshi la Wananchi wa Tanzania na Kijiji cha Lashaine Wilayani Monduli, lakini mwaka 2011 yalifikiwa makubaliano chini ya Mkuu wa Wilaya kuwa mipaka yenye mgogoro isomwe upya kwa kutumia GPS na wananchi wa kijiji cha Lashaine wamekuwa wakisubiri zoezi la kusomwa upya mipaka kwa muda mrefu. Je, Serikali itakamilisha lini makubaliano haya kwa kutumia GPS kusoma mipaka upya ili kumaliza mgogoro huo?

Supplementary Question 2

MHE. DEO K. SANGA: Mheshimiwa Spika, suala la Monduli linafanana na suala la Makambako.
Mheshimiwa Spika, Makambako kuna eneo linaloitwa Kipagamo ambalo miaka ya huko nyuma wananchi waliipa Jeshi kwa ajili ya matumizi ya shabaha. Maeneo hayo sasa tayari wananchi tumejenga shule na tayari kuna makazi ya watu na matumizi hayo sasa hayatumiki kama ambavyo yalivyokuwa yamekusudiwa huko nyuma kwa sababu pana shule na makazi ya watu.
Je, Serikali haioni sasa iko haja ya kuwarudishia wananchi eneo lile ili liendelee kutumika kwa shule na makazi ya watu na kwa sababu barua tulishaiandika kupitia Serikali ya Kijiji na nilimpa mwenyewe Waziri mkono kwa mkono, je, ni lini sasa Serikali itarudisha eneo hilo hilo liendelee kutumika kwa wananchi? Nakushukuru. (Makofi)

Name

Dr. Hussein Ali Mwinyi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kwahani

Answer

WAZIRI WA ULINZI NA JESHI LA KUJENGA TAIFA: Mheshimiwa Spika, kwanza nikiri kwamba barua hiyo Mheshimiwa Mbunge alinikabidhi na nimeipokea na mimi nilichofanya ni kuipeleka Makao Makuu ya Jeshi ili wanipe maoni juu ya suala hilo. Ikumbukwe tu kwamba maeneo yaliyotolewa kwa ajili ya Jeshi yalipangiwa kazi za Jeshi, kwa hiyo inawezekana kwamba eneo hili sasa hivi halitumiki tena kwa shabaha kutokana na ukaribu wake na makazi ya watu lakini huenda linashughuli nyingine za kijeshi.
Mheshimiwa Spika, namuomba Mheshimiwa Mbunge na wananchi wa hapo wavute subira tupate maoni ya Jeshi kuhusu eneo hili, ili hatua stahiki ziweze kuchukuliwa na ni imani yangu kwamba maoni hayo nitayapata muda siyo mrefu. (Makofi)

Name

Masoud Abdalla Salim

Sex

Male

Party

CUF

Constituent

Mtambile

Primary Question

MHE. CECILIA D. PARESSO (K.n.y. MHE. JULIUS K. LAIZER) aliuliza:- Kwa muda mrefu kumekuwa na mgogoro wa mipaka kati ya Jeshi la Wananchi wa Tanzania na Kijiji cha Lashaine Wilayani Monduli, lakini mwaka 2011 yalifikiwa makubaliano chini ya Mkuu wa Wilaya kuwa mipaka yenye mgogoro isomwe upya kwa kutumia GPS na wananchi wa kijiji cha Lashaine wamekuwa wakisubiri zoezi la kusomwa upya mipaka kwa muda mrefu. Je, Serikali itakamilisha lini makubaliano haya kwa kutumia GPS kusoma mipaka upya ili kumaliza mgogoro huo?

Supplementary Question 3

MHE. MASOUD ABDALLAH SALIM: Mheshimiwa Spika, nakushukuru kunipa nafasi ya kuuliza swali moja dogo la nyongeza.
Mheshimiwa Spika, taarifa ya utekelezaji wa ahadi za Serikali mwaka 2006 (miaka kumi iliyopita), Serikali iliahidi kuyapima, kutathmini na kutoa fidia maeneo kadhaa na ndani ya maelezo hayo maeneo yote mliyaeleza mkaainisha katika kitabu ambacho mlitupatia.
Swali linakuja, inakuwaje leo ndani ya muda wa miaka kumi Serikali haijaona umuhimu, ahadi zenu ambazo mlituambia maeneo hayo mtayapima, kutathmini na kutoa fidia na baadhi ya wameshakufa katika maeneo hayo; je, Serikali ina nia njema kulipa fidia wananchi hao? (Makofi)

Name

Dr. Hussein Ali Mwinyi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kwahani

Answer

WAZIRI WA ULINZI NA JESHI LA KUJENGA TAIFA: Mheshimiwa Spika, kama nilivyosema awali na kama alivyosema Mheshimiwa Mbunge, ni kweli kwamba tumeorodhesha maeneo yote yenye migogoro na tumeyaorodhesha maelezo ya nini kinachohitaji kufanyika. Yapo maeneo ambayo yanahitaji kwanza kufanyiwa tathmini ya fidia, yapo yanayohitaji kupimwa, yapo yanayohitaji kutolewa fidia lakini yako vilevile kama nilivyosema awali yale ambayo wananchi walivamia na hawastahili kuwa hapo. Na ukweli wa mambo ni kwamba fedha zinazohitajika ni nyingi, kila mwaka tumekuwa tukitenga katika bajeti yetu, fedha kiasi fulani ili kupunguza awamu kwa awamu mpaka tumalize. Kwa bahati mbaya sana kama mnavyofahamu Waheshimiwa Wabunge ni kwamba fidia ni gharama kubwa. Mheshimiwa Spika, maeneo mengi wananchi wamejenga na kila nyumba ina thamani yake, kwa hiyo kuweza kulimaliza hili tatizo haraka ni vigumu kwasababu ya uwezo wenyewe wa kifedha. Tunachoweza kuendelea kusema ni kwamba kila mwaka, mwaka huu wa fedha tumetenga shilingi bilioni 12, zikipatikana tutaanza sehemu moja baada ya nyingine ili kuweza kuondoa hili tatizo la muda mrefu. Mara nyingi nimekuwa nikisimama hapa nikijibu suala la migogoro ya ardhi kati ya Jeshi na Wananchi lakini ningependa kutoa wito vilevile kwa Waheshimiwa Wabunge kwamba tusaidiane.
Mheshimiwa Spika, zamani Jeshi lilikuwa lina maeneo makubwa sana. Kwa sababu ya uhaba wa ardhi, wananchi sasa hivi wamekuwa wakivamia maeneo hayo. Kwa hiyo, yale maeneo yote ya Jeshi yaliyovamiwa ambayo wananchi hawastahili kuwa hapo ni vema wakatoka katika maeneo hayo na sisi kama Serikali, wale ambao wanastahili ya kulipwa fidia tutaendelea kuwalipa kadri uwezo utakavyokuwa unaruhusu.