Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 19 Sitting 3 Works and Transport Wizara ya Uchukuzi 38 2025-04-10

Name

Antipas Zeno Mngungusi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Malinyi

Primary Question

MHE. DKT. CHRISTINE G. ISHENGOMA K.n.y. MHE. ANTIPAS Z. MGUNGUSI aliuliza:-

Je, Serikali ipo tayari kutenga fedha za ujenzi wa kilometa chache za Barabara ya Lupiro, Malinyi, Kilosa kwa Mpepo na Namtumbo ambayo ni ya Ilani ya CCM?

Name

David Mwakiposa Kihenzile

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mufindi Kusini

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI alijibu:-

Mheshimiwa Naibu Spika, Serikali tayari imesaini mkataba wa ujenzi kwa kiwango cha lami kwa utaratibu wa Sanifu na Jenga kwa sehemu ya Ifakara – Lupiro – Mtimbira yenye urefu wa kilometa 112 ikiwa ni sehemu ya barabara kutoka Kidatu – Ifakara – Lupiro – Malinyi – Kilosa kwa Mpepo – Londo hadi Lumecha Mkoa wa Ruvuma ambapo hiyo barabara yote kwa ujumla wake ina kilometa 435.8 kwa kiwango cha lami. Ahsante. (Makofi)