Bunge la Tanzania
Jamhuri ya Muungano ya Tanzania
Term | Session | Sitting | Sector | Ministry | Qn No | Date |
---|---|---|---|---|---|---|
2020-2025 | Session 19 | Sitting 6 | Regional Administration and Local Government Authorities | Ofisi ya Rais TAMISEMI. | 69 | 2025-04-15 |
Name
Nashon William Bidyanguze
Sex
Male
Party
CCM
Constituent
Kigoma Kusini
Primary Question
MHE. NASHON W. BIDYANGUZE aliuliza:-
Je, lini Serikali itapeleka fedha za kujenga majengo katika Kituo cha Afya Kazuramimba - Uvinza?
Name
Dr. Festo John Dugange
Sex
Male
Party
CCM
Constituent
Wanging'ombe
Answer
NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DKT. FESTO J. DUGANGE) alijibu:-
Mheshimiwa Mwenyekiti, Kituo cha afya Kazuramimba katika Halmashauri ya Uvinza kinahudumia wananchi wapatao 40,711.
Mheshimiwa Mwenyekiti, katika mwaka wa fedha 2024/2025 Serikali imetenga shilingi milioni 625 kwa ajili ya ujenzi wa jengo la wazazi, jengo la upasuaji, jengo la maabara, jengo la kuhifadhi maiti na kichomea taka katika Kituo cha Afya Kazuramimba katika Halmashauri ya Wilaya ya Uvinza. Ahsante.
Copyright © Bunge Polis 2025. All Rights Reserved