Bunge la Tanzania
Jamhuri ya Muungano ya Tanzania
Term | Session | Sitting | Sector | Ministry | Qn No | Date |
---|---|---|---|---|---|---|
2020-2025 | Session 19 | Sitting 6 | Regional Administration and Local Government Authorities | Ofisi ya Rais TAMISEMI. | 70 | 2025-04-15 |
Name
Mrisho Mashaka Gambo
Sex
Male
Party
CCM
Constituent
Arusha Mjini
Primary Question
MHE. MRISHO M. GAMBO aliuliza:-
Je, lini Serikali itaanza na kumaliza ujenzi wa stendi ya kisasa ya Jiji la Arusha katika eneo la Bondeni City?
Name
Dr. Festo John Dugange
Sex
Male
Party
CCM
Constituent
Wanging'ombe
Answer
NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DKT. FESTO J. DUGANGE) alijibu:-
Mheshimiwa Mwenyekiti, Halmashauri ya Jiji la Arusha ni miongoni mwa Miji 45 wanufaika wa Mradi wa Uboreshaji wa Miundombinu ya Miji ya Tanzania (TACTIC). Jiji hili lipo katika kundi la kwanza ya utekelezaji yenye Miji 12 ambapo tayari miradi ya awamu ya kwanza ya barabara na mitaro yenye thamani ya takriban shilingi bilioni 20 ilianza kutekelezwa kwa kusaini mikataba ya Ujenzi Septemba, 2023.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kukosekana kwa wakandarasi wenye vigezo kupitia zabuni zilizotangazwa Machi, 2024, katika miji minne ikiwemo Halmashauri ya Jiji la Arusha, Serikali imetangaza zabuni ya kumpata mkandarasi kwa mara ya pili (Re-advertisement) tarehe 11 Machi, 2025. Mchakato huu unatarajiwa kukamilika mwishoni mwa Aprili, 2025 ambapo mshindi atatangazwa.
Mheshimiwa Mwenyekiti, utekelezaji unatarajiwa kuanza mwezi Mei, 2025 ambapo ujenzi huu unatarajiwa kuwa wa mwaka mmoja na unatarajiwa kukamilika ifikapo Mei, 2026. Ahsante.
Copyright © Bunge Polis 2025. All Rights Reserved