Bunge la Tanzania
Jamhuri ya Muungano ya Tanzania
Term | Session | Sitting | Sector | Ministry | Qn No | Date |
---|---|---|---|---|---|---|
2020-2025 | Session 19 | Sitting 6 | Home Affairs | Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi | 73 | 2025-04-15 |
Name
Abdi Hija Mkasha
Sex
Male
Party
CCM
Constituent
Micheweni
Primary Question
MHE. ABDI HIJA MKASHA aliuliza:-
Je, Kamera zilizofungwa Mji Mkongwe Zanzibar zinasaidiaje katika kupambana na kudhibiti uhalifu kwenye maeneo haya?
Name
Daniel Baran Sillo
Sex
Male
Party
CCM
Constituent
Babati Vijijini
Answer
NAIBU WAZIRI WA MAMBO YA NDANI YA NCHI alijibu:-
Mheshimiwa Mwenyekiti, katika Mji Mkongwe Zanzibar zimewekwa kamera na zilianza kufanya kazi kuanzia tarehe 3 Oktoba, 2018. Matumizi na usimamizi wake unaratibiwa na Ofisi ya Rais, Tawala za Mikoa, Serikali za Mitaa na Idara Maalum za Serikali ya Mapinduzi Zanzibar. Lengo la kuwekwa kamera ni kudhibiti uhalifu na kufuatilia matukio ya kihalifu yanayotendeka. Katika kipindi cha kuanzia mwaka 2018 hadi 2025 kamera hizo zimesaidia kutambua, kufuatilia na kukamatwa matukio 1,177 ya uhalifu. Uwepo wa kamera hizo, umesaidia sana kudhibiti uhalifu na matukio ya kihalifu katika maeneo ya mji Mkongwe. Ahsante.
Copyright © Bunge Polis 2025. All Rights Reserved