Bunge la Tanzania
Jamhuri ya Muungano ya Tanzania
Name
Abdi Hija Mkasha
Sex
Male
Party
CCM
Constituent
Micheweni
Primary Question
MHE. ABDI HIJA MKASHA aliuliza:- Je, Kamera zilizofungwa Mji Mkongwe Zanzibar zinasaidiaje katika kupambana na kudhibiti uhalifu kwenye maeneo haya?
Supplementary Question 1
MHE. ABDI HIJA MKASHA: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante sana kwa majibu mazuri ya Serikali, lakini nina swali dogo moja la nyongeza. Je, ni lini Serikali itafunga kamera za usalama katika Miji ya Pemba ikiwemo na Wilaya ya Micheweni? (Makofi)
Name
Daniel Baran Sillo
Sex
Male
Party
CCM
Constituent
Babati Vijijini
Answer
NAIBU WAZIRI WA MAMBO YA NDANI YA NCHI: Mheshimiwa Mwenyekiti, ninaomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Abdi Hija Mkasha, kama ifuatavyo:-
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa sasa kwa upande wa Pemba, tayari kamera zimeshafungwa kwenye Mji wa Chakechake, Mkoani pamoja na Wete. Vilevile, katika Mwaka wa Fedha 2025/2026, tumetenga fedha kwa ajili ya kumalizia maeneo yaliyobaki ikiwepo Mji wa Micheweni.
Copyright © Bunge Polis 2025. All Rights Reserved