Bunge la Tanzania
Jamhuri ya Muungano ya Tanzania
Term | Session | Sitting | Sector | Ministry | Qn No | Date |
---|---|---|---|---|---|---|
2020-2025 | Session 19 | Sitting 6 | Works and Transport | Wizara ya Ujenzi | 74 | 2025-04-15 |
Name
Ally Mohamed Kassinge
Sex
Male
Party
CCM
Constituent
Kilwa Kusini
Primary Question
MHE. ALLY M. KASSINGE aliuliza:-
Je, nini mpango wa kujenga kwa kiwango cha lami Barabara ya Kiranjeranje – Nanjirinji hadi Ruangwa kwa kuanza kipande cha Kiranjeranje – Makangaga?
Name
Eng. Godfrey Msongwe Kasekenya
Sex
Male
Party
CCM
Constituent
Ileje
Answer
NAIBU WAZIRI WA UJENZI alijibu:-
Mheshimiwa Mwenyekiti, Serikali imeanza ujenzi wa Barabara ya Kiranjeranje – Makangaga – Nanjirinji hadi Ruangwa yenye urefu wa kilometa 120 kwa kuanza na ujenzi wa madaraja makubwa matatu (3) kwa kutumia fedha za dharura zilizotoka kwenye mkopo nafuu wa Benki ya Dunia. Madaraja haya ni Kigombo lenye urefu wa mita 25, utekelezaji wake umefikia 25%, Daraja la Nakiu lenye urefu wa mita 70, kandarasi yake ipo kwenye maandalizi ya ujenzi na Daraja la Mbwemkuru III lenye urefu wa mita 100 lipo katika hatua ya mapitio ya usanifu.
Mheshimiwa Mwenyekiti, wakati ujenzi wa madaraja haya matatu unaendelea, Serikali inaendelea kutafuta fedha ili kujenga barabara hiyo kwa kiwango cha lami. Ahsante.
Copyright © Bunge Polis 2025. All Rights Reserved