Bunge la Tanzania
Jamhuri ya Muungano ya Tanzania
Term | Session | Sitting | Sector | Ministry | Qn No | Date |
---|---|---|---|---|---|---|
2020-2025 | Session 19 | Sitting 6 | Works and Transport | Wizara ya Uchukuzi | 75 | 2025-04-15 |
Name
Dr. Angeline Sylvester Lubala Mabula
Sex
Female
Party
CCM
Constituent
Ilemela
Primary Question
MHE. DKT. ANGELINE S. L. MABULA aliuliza:-
Je, lini ATCL itaanzisha usafiri wa Ndege kutoka Dodoma – Mwanza - Mbeya na Arusha ili kupunguza gharama kwa wasafiri wanaokwenda mikoa hiyo?
Name
David Mwakiposa Kihenzile
Sex
Male
Party
CCM
Constituent
Mufindi Kusini
Answer
NAIBU WAZIRI WA UCHUKUZI alijibu:-
Mheshimiwa Mwenyekiti, ATCL inaendelea kupanua mtandao wa safari kwa kuzingatia mpango mkakati wake na mahitaji ya soko. Kwa sasa, ATCL inahudumia vituo 26 kutokea Dar es Salaam vikiwemo vituo 14 vya ndani ya nchi. Safari za Dodoma – Mwanza zinatarajiwa kuanza Desemba 2025, huku tathmini ikiendelea kwa safari za Dodoma – Mbeya na Dodoma – Arusha.
Copyright © Bunge Polis 2025. All Rights Reserved