Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 19 Sitting 6 Works and Transport Wizara ya Uchukuzi 75 2025-04-15

Name

Dr. Angeline Sylvester Lubala Mabula

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Ilemela

Primary Question

MHE. DKT. ANGELINE S. L. MABULA aliuliza:-

Je, lini ATCL itaanzisha usafiri wa Ndege kutoka Dodoma – Mwanza - Mbeya na Arusha ili kupunguza gharama kwa wasafiri wanaokwenda mikoa hiyo?

Name

David Mwakiposa Kihenzile

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mufindi Kusini

Answer

NAIBU WAZIRI WA UCHUKUZI alijibu:-
Mheshimiwa Mwenyekiti, ATCL inaendelea kupanua mtandao wa safari kwa kuzingatia mpango mkakati wake na mahitaji ya soko. Kwa sasa, ATCL inahudumia vituo 26 kutokea Dar es Salaam vikiwemo vituo 14 vya ndani ya nchi. Safari za Dodoma – Mwanza zinatarajiwa kuanza Desemba 2025, huku tathmini ikiendelea kwa safari za Dodoma – Mbeya na Dodoma – Arusha.