Bunge la Tanzania
Jamhuri ya Muungano ya Tanzania
Term | Session | Sitting | Sector | Ministry | Qn No | Date |
---|---|---|---|---|---|---|
2020-2025 | Session 19 | Sitting 6 | Finance | Wizara ya Fedha | 76 | 2025-04-15 |
Name
Neema Kichiki Lugangira
Sex
Female
Party
CCM
Constituent
Special Seats
Primary Question
MHE. NEEMA K. LUGANGIRA aliuliza: -
Je, hatua gani zimechukuliwa kupunguza makali ya mabadiliko ya sera za nje katika masuala ya fedha za maendeleo kimataifa kwa mataifa yaliyoendelea?
Name
Dr. Mwigulu Lameck Nchemba Madelu
Sex
Male
Party
CCM
Constituent
Iramba Magharibi
Answer
WAZIRI WA FEDHA alijibu:-
Mheshimiwa Spika, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Mbunge Neema Lugangira, kama ifuatavyo:-
Mheshimiwa Mwenyekiti, Serikali imekamilisha tathmini ya athari zitakazojitokeza kwa miradi ambayo ilikuwa ikipata ufadhili kupitia Serikali ya Marekani. Maeneo yaliyoathirika kwa kiasi kikubwa ni pamoja na Sekta ya Afya. Aidha, miradi mikubwa iliyokuwa inagharamiwa kupitia mshirika huyo imetengewa bajeti kupitia fedha za ndani.
Mheshimiwa Spika, Serikali inaendelea na tathmini kwa maeneo mengine yanayoweza kuathirika kwa kiasi kikubwa kutokana na mabadiliko ya sera hizo za nje katika masuala ya fedha kwa kuangalia washirika wengine wa maendeleo ambao Serikali ya Marekani imekuwa ikitoa mchango wao.
Copyright © Bunge Polis 2025. All Rights Reserved