Bunge la Tanzania
Jamhuri ya Muungano ya Tanzania
Term | Session | Sitting | Sector | Ministry | Qn No | Date |
---|---|---|---|---|---|---|
2020-2025 | Session 19 | Sitting 6 | Industries and Trade | Wizara ya Viwanda na Biashara | 78 | 2025-04-15 |
Name
Tunza Issa Malapo
Sex
Female
Party
CHADEMA
Constituent
Special Seats
Primary Question
MHE. ESTHER N. MATIKO K.n.y MHE. TUNZA I. MALAPO aliuliza:-
Je, kuna mkakati gani wa kujenga viwanda vya kuchakata chumvi Mkoani Mtwara?
Name
Dr. Selemani Said Jafo
Sex
Male
Party
CCM
Constituent
Kisarawe
Answer
NAIBU WAZIRI WA MADINI K.n.y WAZIRI WA VIWANDA NA BIASHARA alijibu:-
Mheshimiwa Spika, kwa niaba ya Waziri wa Viwanda na Biashara, ninaomba kujibu swali la Mheshimiwa Tunza Issa Malapo kama ifuatavyo:-
Mheshimiwa Mwenyekiti, Serikali inaendelea kutekeleza Mkakati wa Ujenzi wa Viwanda nchini ikiwemo viwanda vya chumvi. Mkakati huo unahusisha uboreshaji wa mazingira ya biashara na uwekezaji, utengenezaji wa maeneo ya biashara na viwanda na uhamasishaji wa uongezaji wa thamani kwa bidhaa/malighafi kote nchini ikiwemo Mkoa wa Mtwara.
Mheshimiwa Spika, kwa kuzingatia kuwa Mikoa ya Lindi na Mtwara haikuwa na Kiwanda cha Kuchakata Chumvi, Serikali kupitia Shirika la Madini la Taifa (STAMICO) inaendelea na ujenzi wa Kiwanda cha Kuchakata Chumvi Mkoani Lindi. Kiwanda hicho kitakapokamilika kitakuwa kinapokea chumvi ghafi kutoka kwa wazalishaji wadogo wakiwemo wa Mkoa wa Mtwara. Aidha, Serikali kupitia SIDO inaendelea kubuni teknolojia rahisi za kuchakata chumvi ikiwemo kusaga na kurutubisha chumvi kwa ajili ya kusaidia masuala ya lishe. Ahsante sana.
Copyright © Bunge Polis 2025. All Rights Reserved