Bunge la Tanzania
Jamhuri ya Muungano ya Tanzania
Term | Session | Sitting | Sector | Ministry | Qn No | Date |
---|---|---|---|---|---|---|
2020-2025 | Session 19 | Sitting 6 | Industries and Trade | Wizara ya Viwanda na Biashara | 79 | 2025-04-15 |
Name
Condester Michael Sichalwe
Sex
Female
Party
CCM
Constituent
Momba
Primary Question
MHE. CONDESTER M. SICHALWE aliuliza:-
Je, Mitambo mingapi ya kutengeneza Gongo imesambazwa kwa wananchi wanaojishughulisha na uzalishaji wa pombe ya gongo?
Name
Dr. Selemani Said Jafo
Sex
Male
Party
CCM
Constituent
Kisarawe
Answer
NAIBU WAZIRI WA MADINI K.n.y. WAZIRI WA VIWANDA NA BIASHARA alijibu:-
Mheshimiwa Spika, mpaka sasa viwanda vya kutengeneza pombe kali nchini inayokidhi viwango, vinaendelea kuanzishwa kwa kupata mafunzo na ushauri wa kitaalam kutoka Shirika la Maendeleo ya Viwanda Vidogo (SIDO), Mamlaka ya Maabara ya Mkemia Mkuu wa Serikali (GCLA) na Shirika la Viwango Tanzania (TBS) na miongoni mwao wako watengenezaji wanaoendelea kupata alama ya ubora kwa kukidhi vigezo.
Mheshimiwa Spika, SIDO itaendelea kushirikiana na taasisi nyingine za maendeleo ya teknolojia ikiwemo Taasisi ya Uhandisi na Usanifu Mitambo (TEMDO), Kituo cha Zana za Kilimo na Teknolojia Vijijini (CAMARTEC) na kwa ushirikiano wa karibu wa Mamlaka ya Maabara ya Mkemia Mkuu wa Serikali (GCLA) na Shirika la Viwango Tanzania (TBS), kwa kuboresho teknolojia za kuchakata pombe kali kwa teknolojia rahisi ili watengenezaji wengi waweze kutengeneza pombe bora inayostahili kwa matumizi ya binadamu.
Mheshimiwa Spika, gongo ni pombe yenye kilevi ambayo imekuwa ikitengenezwa kienyeji. Aidha, Serikali haijahalalisha pombe ya gongo kwa sababu ya kuwa na madhara makubwa katika mwili wa binadamu. Kwa msingi huo, mpaka sasa hakuna mitambo ya kutengeneza kinywaji hicho iliyosambazwa kwa wananchi. Kwa sasa, Serikali haijaanzisha mpango wa kusambaza mitambo ya gongo kwa wananchi wanaojishughulisha na uzalishaji wa pombe ya gongo. Ahsante sana. (Makofi)
Copyright © Bunge Polis 2025. All Rights Reserved