Bunge la Tanzania
Jamhuri ya Muungano ya Tanzania
Term | Session | Sitting | Sector | Ministry | Qn No | Date |
---|---|---|---|---|---|---|
2020-2025 | Session 19 | Sitting 6 | Livestock , Fisheries, Agriculture, Food Security and Cooperatives | Waziri wa Mifugo na Uvuvi | 81 | 2025-04-15 |
Name
Boniphace Mwita Getere
Sex
Male
Party
CCM
Constituent
Bunda
Primary Question
MHE. ESTER A. BULAYA K.n.y. MHE. BONIPHACE M. GETERE aliuliza:-
Je, lini Serikali itakamilisha ahadi ya ujenzi wa Mnada wa Mifugo Mngeta, Bunda?
Name
Alexander Pastory Mnyeti
Sex
Male
Party
CCM
Constituent
Misungwi
Answer
NAIBU WAZIRI WA MIFUGO NA UVUVI alijibu:-
Mheshimiwa Mwenyekiti, katika mwaka wa fedha 2025/2026, Serikali haikuweka kwenye mpango ujenzi wa minada mipya hapa nchini ili kutoa fursa ya ukamilishwaji wa minada 23 ya awali iliyopo katika hatua mbalimbali za ujenzi. Serikali ina jukumu la moja kwa moja la kujenga na kuendesha minada ya upili na mpakani, hivyo Wizara itaendelea kuweka katika mpango wa bajeti ujenzi wa minada ya awali nchini, ikiwemo mnada wa Mifugo Mngeta kulingana na upatikanaji wa fedha.
Mheshimiwa Mwenyekiti, aidha, katika bajeti ya mwaka 2023/2024, Serikali ilitenga jumla ya shilingi 435,238,870, kwa ajili ya ujenzi wa mnada wa Bitalaguro uliopo katika Halmashauri ya Wilaya ya Bunda. Aidha, Mwezi Februari, 2025 ujenzi wa mnada huo ulikamilika. Hivyo, kukamilika kwa ujenzi wa Mnada wa Bitalaguro utatoa fursa kwa wananchi wa Halmashauri ya Bunda kuuza na kununua mifugo katika mnada huo.
Copyright © Bunge Polis 2025. All Rights Reserved