Bunge la Tanzania
Jamhuri ya Muungano ya Tanzania
Term | Session | Sitting | Sector | Ministry | Qn No | Date |
---|---|---|---|---|---|---|
2020-2025 | Session 19 | Sitting 7 | Regional Administration and Local Government Authorities | Ofisi ya Rais TAMISEMI. | 82 | 2025-04-16 |
Name
Munira Mustafa Khatib
Sex
Female
Party
CCM
Constituent
Special Seats
Primary Question
MHE. MUNIRA MUSTAPHA KHATIB aliuliza: -
Je, Serikali ina mkakati gani wa kuongeza idadi ya madaktari na wauguzi hasa maeneo ya vijijini?
Name
Dr. Festo John Dugange
Sex
Male
Party
CCM
Constituent
Wanging'ombe
Answer
NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DKT. FESTO J. DUGANGE) alijibu: -
Mheshimiwa Spika, Serikali imeendelea kutenga bajeti na kuajiri watumishi wa kada mbalimbali za afya nchini. Katika kipindi cha mwaka wa fedha 2020/2021 – 2024/2025, jumla ya watumishi wa kada mbalimbali za afya 34,720 wameajiriwa. Wataalamu hao ni pamoja na madaktari 1,851; wauguzi 10,213 pamoja na kada nyingine 22,656. Aidha, zaidi ya 70% ya watumishi hawa wamepangiwa kazi kwenye vituo vya maeneo ya vijijini.
Mheshimiwa Spika, Serikali itaendelea kutenga bajeti na kuajiri watumishi wa kada mbalimbali za afya na kuwapanga katika maeneo yenye upungufu hususan vijijini katika Mamlaka za Serikali za Mitaa, ahsante.
Copyright © Bunge Polis 2025. All Rights Reserved