Bunge la Tanzania
Jamhuri ya Muungano ya Tanzania
Term | Session | Sitting | Sector | Ministry | Qn No | Date |
---|---|---|---|---|---|---|
2020-2025 | Session 19 | Sitting 7 | Regional Administration and Local Government Authorities | Ofisi ya Rais TAMISEMI. | 83 | 2025-04-16 |
Name
Ghati Zephania Chomete
Sex
Female
Party
CCM
Constituent
Special Seats
Primary Question
MHE. GHATI Z. CHOMETE aliuliza: -
Je, kwa nini katika Kituo cha Afya Iramba wanawake na watoto wanalazwa katika wodi moja?
Name
Dr. Festo John Dugange
Sex
Male
Party
CCM
Constituent
Wanging'ombe
Answer
NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DKT. FESTO J. DUGANGE) alijibu: -
Mheshimiwa Spika, Kituo cha Afya Iramba katika Halmashauri ya Wilaya ya Serengeti kinahudumia wananchi wapatao 77,027. Serikali inatambua upungufu wa miundombinu katika vituo vya afya, hali inayopelekea baadhi ya vituo kukosa miundombinu ya msingi ikiwemo wodi za kulaza watoto, wanawake na wanaume.
Mheshimiwa Spika, katika mwaka wa fedha 2025/2026 Serikali kupitia mapato ya ndani ya Halmashauri ya Wilaya ya Serengeti imetenga shilingi milioni 75 kwa ajili ya kuanza ujenzi wa wodi ya watoto, wanawake na wanaume katika Kituo cha Afya cha Iramba.
Copyright © Bunge Polis 2025. All Rights Reserved