Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2015-2020 Session 4 Sitting 7 Water and Irrigation Wizara ya Maji 89 2016-09-15

Name

Sikudhani Yasini Chikambo

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. SIKUDHANI Y. CHIKAMBO aliuliza:-
Miradi ya Maji ya Benki ya Dunia nchini imekuwa ikisuasua sana na hata ile iliyokamilika maji yamekuwa yakitoka wakati wa mvua tu.
Je, ni lini Serikali itakamilisha miradi inayosuasua ikiwemo ile ya Wilaya ya Tunduru?

Name

Eng. Isack Aloyce Kamwelwe

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Katavi

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAJI NA UMWAGILIAJI alijibu:-
Mheshimiwa Spika, kwa niaba ya Waziri wa Maji na Umwagiliaji naomba kujibu swali la Mheshimiwa Sikudhani Yassini Chikambo, Mbunge Viti Maalum, kama ifuatavyo:-
Mheshimiwa Spika, Serikali inatekeleza programu ya maendeleo ya sekta ya maji kwa kushirikiana na wadau mbalimbali wa maendeleo. Kasi ndogo ya utekelezaji wa miradi katika Jimbo la Tunduru kama ilivyo pia katika maeneo mengine nchini ilitokana na changamoto ya upatikanaji wa fedha pamoja na kutopatikana kwa vyanzo vya maji vya uhakika katika baadhi ya maeneo.
Mheshimiwa Spika, katika awamu ya kwanza ya utekelezaji wa Programu ya Maendeleo Sekta ya Maji, Halmashauri ya Wilaya ya Tunduru ilipanga kutekeleza jumla ya miradi kumi na moja, kati ya hiyo, miradi minne ya vijiji vya Nandembo, Nalasi, Lukumbule na Amani ujenzi wake unaendelea na miradi minne katika vijiji vya Majimaji, Muhuwesi, Nakapanya na Mchoteka haikupata vyanzo. Aidha, mradi wa Mbesa umesimama baada ya Halmashauri kuvunja mkataba wa mkandarasi kutokana na kutokishi taratibu za kimkataba na tayari taratibu zinaendelea kumpata mkandarasi mwingine.
Mheshimiwa Spika, miradi yote ambayo haikupata vyanzo itapewa kipaumbele katika Awamu ya Pili ya utekelezaji wa Programu ya Maendeleo ya Sekta ya Maji iliyoanza mwezi Januari, 2016.
Mheshimiwa Spika, katika kuhakikisha miradi hiyo inakamilika, mwezi Agosti, 2016 Wizara imetuma kiasi cha shilingi milioni 147.4 kwa Halmashauri ya Tunduru na Serikali itaendelea kutuma fedha kwa kadri zitakavyopatikana. Upungufu wa maji kwenye miradi iliyokamilika hususan wakati wa kiangazi umesababishwa na mabadiliko ya tabianchi pamoja na uharibifu wa mazingira unaosababishwa na shughuli za kibinadamu. Wizara inashauri tuendelee kuihamasisha jamii katika uhifadhi wa mazingira na utunzaji wa vyanzo vya maji.