Bunge la Tanzania
Jamhuri ya Muungano ya Tanzania
Term | Session | Sitting | Sector | Ministry | Qn No | Date |
---|---|---|---|---|---|---|
2020-2025 | Session 19 | Sitting 7 | Regional Administration and Local Government Authorities | Ofisi ya Rais TAMISEMI. | 85 | 2025-04-16 |
Name
Rehema Juma Migilla
Sex
Female
Party
CCM
Constituent
Ulyankulu
Primary Question
MHE. OMARI M. KIGUA K.n.y. MHE. REHEMA J. MIGILLA aliuliza:-
Je, lini Serikali itafanya ukarabati wa Shule za Msingi Taba, Mkindo, Kaswa, Mbeta na Milambo?
Name
Zainab Athuman Katimba
Sex
Female
Party
CCM
Constituent
Special Seats
Answer
NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. ZAINAB A. KATIMBA) alijibu: -
Mheshimiwa Spika, mwaka 2024/2025 Serikali ilitoa shilingi milioni 380 kwa ajili ya ukarabati wa miundombinu ya Shule za Msingi za Seleli, Makingi, Ntyemo, Kagunga, Kabanga, Unampanda na Kashishi za Halmashauri ya Wilaya ya Kaliua. Katika mpango na bajeti ya mwaka 2025/2026 Serikali inatarajia kutumia shilingi milioni 270 kwa ajili ya ukarabati wa miundombinu ya shule za msingi 10 zikiwemo Shule za Milambo, Ichemba, Kaswa, Mbeta, Taba na Mkindo. Serikali itaendelea kutenga fedha ya ukarabati wa miundombinu ya shule chakavu zikiwemo Shule za Msingi Taba, Mkindo na Milambo kadiri ya upatikanaji wa fedha.
Copyright © Bunge Polis 2025. All Rights Reserved