Bunge la Tanzania
Jamhuri ya Muungano ya Tanzania
Term | Session | Sitting | Sector | Ministry | Qn No | Date |
---|---|---|---|---|---|---|
2020-2025 | Session 19 | Sitting 7 | Good Governance | Ofisi ya Rais (Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora) | 87 | 2025-04-16 |
Name
Dr. Alice Karungi Kaijage
Sex
Female
Party
CCM
Constituent
Special Seats
Primary Question
MHE. DKT. ALICE K. KAIJAGE aliuliza: -
Je, Serikali ina mpango gani wa kufuatilia waajiri ili wawe wanatoa mafunzo kwa watumishi kabla ya kustaafu?
Name
Deus Clement Sangu
Sex
Male
Party
CCM
Constituent
Kwela
Answer
NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, MENEJIMENTI YA UTUMISHI WA UMMA NA UTAWALA BORA alijibu: -
Mheshimiwa Spika, Serikali imetoa maelekezo kwa waajiri kupitia Kanuni G.1(7) ya Kanuni za Kudumu katika Utumishi wa Umma za mwaka 2009, kuhakikisha wanaandaa mipango ya mafunzo kwa watumishi na kufanya tathmini ya mahitaji ya mafunzo (training need assessment), kutenga bajeti na kusimamia utekelezaji wake. Katika kutekeleza maelekezo hayo, kwa kipindi cha mwaka 2022/2023 hadi mwaka 2024/2025, jumla ya watumishi 3,036 kutoka kwa waajiri mbalimbali walipatiwa mafunzo kabla ya kustaafu katika Chuo cha Utumishi wa Umma. Hata hivyo, Serikali itaendelea kuwasisitiza waajiri kuhakikisha suala la mafunzo kwa watumishi kabla ya kustaafu linapewa kipaumbele katika utumishi wa umma, ninakushukuru.
Copyright © Bunge Polis 2025. All Rights Reserved